-
Ufunuo 14:9, 10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Malaika mwingine, wa tatu, akawafuata, akisema kwa sauti kubwa: “Yeyote akimwabudu yule mnyama wa mwituni+ na sanamu yake na kupokea alama kwenye paji la uso wake au kwenye mkono wake,+ 10 yeye pia atakunywa divai ya hasira ya Mungu inayomwagwa ndani ya kikombe cha ghadhabu Yake bila kuchanganywa na kitu,+ naye atateswa kwa moto na kiberiti+ machoni pa malaika watakatifu na machoni pa Mwanakondoo.
-
-
Ufunuo 19:20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
20 Na yule mnyama wa mwituni akakamatwa, na yule nabii+ wa uwongo pamoja naye, aliyefanya mbele yake ishara alizotumia kuwapotosha wale waliopokea alama ya yule mnyama wa mwituni+ na wale wanaoiabudu sanamu yake.+ Wakiwa bado hai, wote wawili walitupwa ndani ya ziwa la moto linalowaka kwa kiberiti.+
-