-
Waroma 4:11, 12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Naye alipokea ishara+—yaani, kutahiriwa—kuwa muhuri wa* uadilifu kwa imani aliyokuwa nayo alipokuwa katika hali yake ya kutotahiriwa, ili awe baba ya wale wote walio na imani+ ingawa hawajatahiriwa, kusudi wahesabiwe kuwa waadilifu; 12 na ili awe baba ya uzao uliotahiriwa, si kwa wale tu wanaoshikamana na kutahiriwa, bali pia kwa wale wanaotembea kwa utaratibu katika hatua za imani ambayo baba yetu Abrahamu+ alikuwa nayo katika hali ya kutotahiriwa.
-