-
1 Wakorintho 6:9-11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Au je, hamjui kwamba watu wasio waadilifu hawataurithi Ufalme wa Mungu?+ Msipotoshwe.* Waasherati,*+ waabudu-sanamu,+ wazinzi,+ wanaume wanaofanya ngono na wanaume,*+ 10 wezi, watu wenye pupa,+ walevi,+ watukanaji,* na wanyang’anyi hawataurithi Ufalme wa Mungu.+ 11 Na bado baadhi yenu mlikuwa hivyo. Lakini mmeoshwa mkawa safi;+ mmetakaswa;+ mmetangazwa kuwa waadilifu+ katika jina la Bwana Yesu Kristo na kwa roho ya Mungu wetu.
-
-
Tito 3:3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Kwa maana hata sisi wakati mmoja tulikuwa watu wasio na akili, wasiotii, waliopotoshwa, watumwa wa tamaa na anasa mbalimbali, tukiendeleza ubaya na wivu, tukiwa wenye kuchukiza, na kuchukiana.
-