-
2 Timotheo 2:16-18Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
16 Lakini kataa maneno matupu ambayo huchafua mambo matakatifu,+ kwa maana yataongoza kwenye kutomwogopa Mungu zaidi na zaidi, 17 na neno lao litaenea kama kidonda kinachooza. Himenayo na Fileto ni kati yao.+ 18 Watu hao wamegeuka kutoka kwenye kweli, wakisema kwamba tayari ufufuo umetukia,+ nao wanapindua imani ya wengine.
-
-
1 Yohana 2:18, 19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 Watoto wadogo, ni saa ya mwisho, na kama vile mlivyosikia kwamba mpinga-Kristo anakuja,+ hata sasa wapinga-Kristo wengi wametokea,+ na kwa sababu hiyo tunajua kwamba ni saa ya mwisho. 19 Waliondoka miongoni mwetu, lakini hawakuwa wa namna yetu;*+ kwa maana kama wangekuwa wa namna yetu, wangebaki pamoja nasi. Lakini waliondoka ili ionekane kwamba si wote walio wa namna yetu.+
-