-
Kutoka 24:6-8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Kisha Musa akachukua nusu ya damu ya wanyama hao na kuitia ndani ya mabakuli, na nusu ya damu hiyo akainyunyiza kwenye madhabahu. 7 Halafu akachukua kitabu cha agano na kuwasomea watu kwa sauti.+ Nao wakasema: “Mambo yote ambayo Yehova amesema tuko tayari kuyafanya, nasi tutatii.”+ 8 Basi Musa akachukua damu akawanyunyizia watu+ na kusema: “Hii ndiyo damu ya agano ambalo Yehova amefanya pamoja nanyi kulingana na maneno hayo yote.”+
-