9 Mwishowe wakafika mahali ambapo Mungu wa kweli alikuwa amemwonyesha, Abrahamu akajenga madhabahu hapo na kupanga kuni juu yake. Akamfunga Isaka mwanawe mikono na miguu na kumlaza kwenye madhabahu juu ya zile kuni.+ 10 Kisha Abrahamu akaunyoosha mkono wake na kuchukua kisu ili amuue mwanawe.+