6 Sikilizeni! Kuna mtu anayesema: “Tangaza!”
Mwingine anauliza: “Nitangaze nini?”
“Wote wenye mwili ni majani mabichi.
Upendo wao wote mshikamanifu ni kama ua la shambani.+
7 Majani mabichi hukauka,
Ua hunyauka,+
Kwa sababu pumzi ya Yehova hupuliza juu yake.+
Kwa hakika watu ni majani mabichi tu.
8 Majani mabichi hukauka,
Ua hunyauka,
Lakini neno la Mungu wetu linadumu milele.”+