18 Watoto wadogo, ni saa ya mwisho, na kama vile mlivyosikia kwamba mpinga-Kristo anakuja,+ hata sasa wapinga-Kristo wengi wametokea,+ na kwa sababu hiyo tunajua kwamba ni saa ya mwisho.
3 Lakini kila neno lililoongozwa na roho ambalo halimkiri Yesu halitoki kwa Mungu.+ Zaidi ya hayo, hili ndilo neno lililoongozwa na roho la yule mpinga-Kristo ambalo mmesikia kwamba linakuja,+ na sasa tayari limo ulimwenguni.+
4 Kwa maana watu fulani wameingia kisiri kati yenu ambao Maandiko yalisema tangu zamani kwamba wanastahili hukumu; watu hao hawamwogopi Mungu, wanazitumia fadhili zisizostahiliwa za Mungu wetu kuwa kisingizio cha mwenendo mpotovu*+ wakimkana mmiliki* wetu pekee na Bwana wetu, Yesu Kristo.+