-
Ezekieli 3:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Kisha akaniambia: “Mwana wa binadamu, kula kilicho mbele yako.* Kula kitabu hiki cha kukunjwa, na uende ukazungumze na watu wa nyumba ya Israeli.”+
2 Kwa hiyo nikafungua kinywa changu, naye akanipa kitabu hicho nile. 3 Naye akaendelea kuniambia: “Mwana wa binadamu, kula kitabu hiki ninachokupa, ukijaze tumboni mwako.” Basi nikaanza kukila, nacho kilikuwa kitamu kama asali kinywani mwangu.+
-