-
Ufunuo 10:9, 10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Nikaenda kwa yule malaika na kumwambia anipe kile kitabu kidogo cha kukunjwa. Akaniambia: “Kichukue ukile,+ nacho kitafanya tumbo lako liwe na uchungu, lakini kinywani mwako kitakuwa kitamu kama asali.” 10 Nikakichukua kile kitabu kidogo cha kukunjwa kutoka mkononi mwa yule malaika nikakila,+ na kinywani mwangu kilikuwa kitamu kama asali,+ lakini baada ya kukila, tumbo langu likawa na uchungu.
-