-
Ezekieli 3:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Kisha akaniambia: “Mwana wa binadamu, kula kilicho mbele yako.* Kula kitabu hiki cha kukunjwa, na uende ukazungumze na watu wa nyumba ya Israeli.”+
2 Kwa hiyo nikafungua kinywa changu, naye akanipa kitabu hicho nile. 3 Naye akaendelea kuniambia: “Mwana wa binadamu, kula kitabu hiki ninachokupa, ukijaze tumboni mwako.” Basi nikaanza kukila, nacho kilikuwa kitamu kama asali kinywani mwangu.+
-
-
Ufunuo 10:9, 10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Nikaenda kwa yule malaika na kumwambia anipe kile kitabu kidogo cha kukunjwa. Akaniambia: “Kichukue ukile,+ nacho kitafanya tumbo lako liwe na uchungu, lakini kinywani mwako kitakuwa kitamu kama asali.” 10 Nikakichukua kile kitabu kidogo cha kukunjwa kutoka mkononi mwa yule malaika nikakila,+ na kinywani mwangu kilikuwa kitamu kama asali,+ lakini baada ya kukila, tumbo langu likawa na uchungu.
-