7 Ulisema: “Sikuzote nitakuwa Bimkubwa, milele.”+
Hukutia mambo haya moyoni mwako;
Hukufikiria mwisho wa jambo hilo.
8 Sasa sikia jambo hili, ewe mpenda raha,+
Unayeketi kwa usalama, unayesema moyoni mwako:
“Mimi ndiye, na hakuna mwingine.+
Sitakuwa mjane.
Sitajua kamwe inavyokuwa kupoteza watoto.”+
9 Lakini mambo haya mawili yatakupata ghafla, kwa siku moja:+
Kupoteza watoto na ujane.
Yatakupata kwa kipimo kamili+
Kwa sababu ya ulozi wako mwingi na uchawi wako wenye nguvu.+