Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Mambo ya Nyakati 13
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

1 Mambo ya Nyakati—Yaliyomo

      • Sanduku la agano laletwa kutoka Kiriath-yearimu (1-14)

        • Uza auawa (9, 10)

1 Mambo ya Nyakati 13:1

Marejeo

  • +1Nya 15:25

1 Mambo ya Nyakati 13:2

Marejeo

  • +Hes 35:2

1 Mambo ya Nyakati 13:3

Marejeo

  • +1Sa 7:2
  • +1Sa 14:18

1 Mambo ya Nyakati 13:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kuanzia Shihori huko Misri.”

  • *

    Au “njia ya kuingia Hamathi.”

Marejeo

  • +Hes 34:2, 8
  • +1Sa 6:21-7:1; 2Sa 6:1, 2; 1Nya 15:3

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    The Watchtower,

    10/1/2005, uku. 10

  • Fahirishi ya Machapisho

    w05 10/1 10

1 Mambo ya Nyakati 13:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “katikati ya.”

Marejeo

  • +Yos 15:9, 12
  • +Kut 25:22; Hes 7:89; 1Sa 4:4; 2Sa 6:2

1 Mambo ya Nyakati 13:7

Marejeo

  • +Kut 37:5
  • +2Sa 6:3-8

1 Mambo ya Nyakati 13:8

Marejeo

  • +Kut 15:20
  • +1Nya 25:1
  • +2Nya 5:13

1 Mambo ya Nyakati 13:10

Marejeo

  • +Hes 4:15
  • +Law 10:1, 2

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    The Watchtower,

    2/1/2005, kur. 26-27

  • Fahirishi ya Machapisho

    w05 2/1 26-27

1 Mambo ya Nyakati 13:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Maana yake “Ghadhabu Dhidi ya Uza.”

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    The Watchtower,

    10/1/2005, uku. 11

  • Fahirishi ya Machapisho

    w05 10/1 11

1 Mambo ya Nyakati 13:12

Marejeo

  • +2Sa 6:9-11

1 Mambo ya Nyakati 13:14

Marejeo

  • +Mwa 30:27; 39:5

Tafsiri Mbalimbali

Bofya nambari ya mstari ili kuona mstari huo katika tafsiri mbalimbali za Biblia.

Jumla

1 Nya. 13:11Nya 15:25
1 Nya. 13:2Hes 35:2
1 Nya. 13:31Sa 7:2
1 Nya. 13:31Sa 14:18
1 Nya. 13:5Hes 34:2, 8
1 Nya. 13:51Sa 6:21-7:1; 2Sa 6:1, 2; 1Nya 15:3
1 Nya. 13:6Yos 15:9, 12
1 Nya. 13:6Kut 25:22; Hes 7:89; 1Sa 4:4; 2Sa 6:2
1 Nya. 13:7Kut 37:5
1 Nya. 13:72Sa 6:3-8
1 Nya. 13:8Kut 15:20
1 Nya. 13:81Nya 25:1
1 Nya. 13:82Nya 5:13
1 Nya. 13:10Hes 4:15
1 Nya. 13:10Law 10:1, 2
1 Nya. 13:122Sa 6:9-11
1 Nya. 13:14Mwa 30:27; 39:5
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Soma katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
1 Mambo ya Nyakati 13:1-14

Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati

13 Daudi alishauriana na wakuu wa maelfu na wa mamia na kila kiongozi.+ 2 Kisha Daudi akaliambia kutaniko lote la Waisraeli: “Mkiona ni vema na ikiwa ni jambo linalokubalika kwa Yehova Mungu wetu, acheni tutume ujumbe kwa ndugu zetu waliobaki katika maeneo yote ya Israeli na pia kwa makuhani na Walawi katika majiji yao+ yenye malisho waje kuungana nasi. 3 Na acheni tulirudishe Sanduku+ la Mungu wetu.” Kwa maana hawakuwa wamelitunza katika siku za Sauli.+ 4 Kutaniko lote likakubali kufanya hivyo, kwa maana watu wote waliliona kuwa jambo jema. 5 Basi Daudi akawakusanya Waisraeli wote, kuanzia mto wa Misri* mpaka Lebo-Hamathi,*+ ili walete Sanduku la Mungu wa kweli kutoka Kiriath-yearimu.+

6 Daudi na Waisraeli wote wakapanda kwenda Baala,+ mpaka Kiriath-yearimu, jiji la Yuda, ili kuleta kutoka huko Sanduku la Mungu wa kweli, Yehova, anayeketi kwenye kiti cha ufalme juu ya* makerubi,+ mahali ambapo watu husali katika jina lake. 7 Hata hivyo, walilitoa Sanduku la Mungu wa kweli katika nyumba ya Abinadabu na kuliweka juu ya gari jipya la kukokotwa,+ na Uza na Ahio walikuwa wakiliongoza gari hilo.+ 8 Daudi na Waisraeli wote walikuwa wakisherehekea mbele za Mungu wa kweli kwa nguvu zao zote, kwa nyimbo, vinubi, vinanda vinginevyo, matari,+ matoazi,+ na tarumbeta.+ 9 Lakini walipofika kwenye uwanja wa kupuria wa Kidoni, Uza aliunyoosha mkono wake haraka na kulikamata Sanduku hilo, kwa sababu ng’ombe walikuwa karibu kuliangusha. 10 Ndipo hasira ya Yehova ikawaka dhidi ya Uza, Naye akamuua kwa sababu aliunyoosha mkono wake na kulikamata Sanduku+ hilo, naye akafa hapo mbele za Mungu.+ 11 Lakini Daudi akakasirika kwa sababu hasira kali ya Yehova iliwaka dhidi ya Uza; na tangu siku hiyo mahali hapo panaitwa Peres-uza.*

12 Basi Daudi akamwogopa Mungu wa kweli siku hiyo na kusema: “Ninawezaje kulileta kwangu Sanduku la Mungu wa kweli?”+ 13 Daudi hakulileta Sanduku hilo mahali alipokuwa katika Jiji la Daudi, lakini aliagiza lipelekwe katika nyumba ya Obed-edomu, Mgathi. 14 Sanduku la Mungu wa kweli lilikaa pamoja na watu wa nyumba ya Obed-edomu, likabaki katika nyumba yake kwa miezi mitatu, na Yehova akaendelea kuwabariki watu wa nyumba ya Obed-edomu na vitu vyote alivyokuwa navyo.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki