Zaburi
Kwa kiongozi. Umepatanishwa na muziki wa “Usiharibu.” Wimbo wa Asafu.+
75 Tunakushukuru, Ee Mungu, tunakushukuru;
Jina lako liko karibu,+
Na watu wanatangaza kazi zako zinazostaajabisha.
2 Unasema: “Ninapoweka wakati hususa,
Ninahukumu kwa haki.
3 Dunia na wakaaji wake wote walipoyeyushwa,
Mimi ndiye niliyeziimarisha nguzo zake.” (Sela)
4 Ninawaambia wenye kujigamba, “Msijigambe,”
Na waovu, “Msikweze nguvu zenu.*
6 Kwa maana kukwezwa
Hakutoki mashariki wala magharibi wala kusini.
7 Kwa maana Mungu ni Mwamuzi.+
Humshusha huyu na kumkweza yule.+
Hakika ataimwaga,
Na waovu wote duniani watainywa, mpaka machicha yake.”+
10 Kwa maana anasema: “Nitazikata nguvu* zote za waovu.”
Lakini nguvu* za waadilifu zitakwezwa.