Wimbo wa Sulemani
7 “Miguu yako inapendeza kwelikweli katika viatu vyako,
Ewe binti unayeheshimika!
Umbo la mapaja yako ni kama mapambo,
Kazi ya mikono ya fundi.
2 Kitovu chako ni bakuli la mviringo.
Kisikose kamwe divai iliyotiwa vikolezo.
Tumbo lako ni rundo la ngano,
Lililozungukwa na mayungiyungi.
4 Shingo yako+ ni kama mnara wa pembe ya tembo.+
Pua yako ni kama mnara wa Lebanoni,
Unaoelekea Damasko.
Mfalme ameduwazwa* na nywele zako ndefu.
6 Wewe ni mrembo kwelikweli, nawe unapendeza sana,
Ewe msichana mpendwa, unazidi vyote vinavyopendeza!
8 Nilisema, ‘Nitapanda juu ya mtende
Nishike vitawi vyake vyenye tende.’
Matiti yako na yawe kama vishada vya mizabibu,
Na pumzi yako inanukia kama matofaa,
“Na ishuke taratibu kwa ajili ya mpenzi wangu,
Itiririke taratibu juu ya midomo ya mpenzi wangu.*
12 Tuamke mapema twende kwenye mashamba ya mizabibu
Tuone ikiwa mzabibu umechipuka,
Ikiwa maua yamechanua,+
Ikiwa mikomamanga imechanua.+
Huko nitakuonyesha upendo wangu.+
Mapya na pia ya zamani,
Ewe mpenzi wangu, nimekuhifadhia.