25 Bildadi+ Mshua akajibu:
2 “Utawala na uwezo wenye kutisha ni wake;
Yeye huimarisha amani mbinguni.
3 Je, majeshi yake yanaweza kuhesabiwa?
Ni nani asiyeangaziwa na nuru yake?
4 Basi mwanadamu anayeweza kufa anawezaje kuwa mwadilifu mbele za Mungu,+
Au mtu aliyezaliwa na mwanamke anawezaje kuwa bila hatia?+
5 Hata mwezi si mwangavu
Na nyota si safi machoni pake,
6 Sembuse mwanadamu anayeweza kufa ambaye ni buu,
Na binadamu ambaye ni mnyoo!”