Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 uku. 1957
  • 2 “Gehena”—Hufananisha Uharibifu Kamili

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • 2 “Gehena”—Hufananisha Uharibifu Kamili
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
2 “Gehena”—Hufananisha Uharibifu Kamili

2 “Gehena”—Hufananisha Uharibifu Kamili

Kiebrania, הנם גי (geh hin·nomʹ, “bonde la Hinomu”); Kigiriki, γέεννα (geʹen·na); Kilatini, ge·henʹna

“Gehena” humaanisha “bonde la Hinomu.” Neno hilo ambalo ni la Kigiriki limetafsiriwa kutokana na neno geh hin·nomʹ la Kiebrania. Katika Yos 18:16, ambapo panapatikana maneno “bonde la Hinomu,” katika Septuajinti ya Kigiriki neno “Gehena” limetumiwa. Linapatikana mara 12 katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, linaonekana kwanza katika Mt 5:22. Tafsiri ya Ulimwengu Mpya inatafsiri neno hilo kuwa “Gehena” kila mahali linapoonekana, yaani, katika Mt 5:22, 29, 30; 10:28; 18:9; 23:15, 33; Mk 9:43, 45, 47; Lu 12:5; Yak 3:6.

Bonde la Hinomu lilifanywa kuwa mahali pa kutupa takataka na pa kuteketeza kwa moto uchafu wote wa Yerusalemu. Mizoga ya wanyama waliokufa ilitupwa ndani ili kuteketezwa katika moto, na salfa, au kiberiti, iliongezwa kwenye moto huo, ili kusaidia kuteketeza. Vilevile maiti za ­wahalifu waliouawa zilitupwa humo kwa sababu walionwa kuwa hawastahili kuzikwa kwa heshima kwenye makaburi. Maiti zilizoanguka motoni ziliteketea kabisa, lakini mizoga iliyoanguka kwenye miamba ya poromoko hilo lenye kina kirefu, ilianza kuoza na kuvamiwa na wadudu, au minyoo ambao hawakufa mpaka walipokuwa wamemaliza kula nyama zote na kuacha mifupa tu.

Hakuna mnyama au mwanadamu yeyote aliye hai ambaye alitupwa katika Gehena ili ateketee kwa moto na kuteseka. Kwa hiyo, mahali hapo hapawezi kamwe kufananisha mahali pasipoonekana ambapo nafsi za wanadamu zinateswa milele katika moto halisi au ambapo zinaliwa milele na wadudu ambao hawafi. Wahalifu waliokufa walitupwa humo na hivyo hawakuzikwa kwa heshima kwenye kaburi, linalofananisha tumaini la ufufuo. Ndiyo sababu Yesu na wanafunzi wake walitumia Gehena kuonyesha uharibifu wa milele, kuangamizwa kutoka katika ulimwengu wa Mungu, au “kifo cha pili,” adhabu ya ­milele.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki