Yakobo
3 Si wengi kati yenu wanaopaswa kuwa walimu,+ ndugu zangu, mkijua kwamba tutapokea hukumu nzito zaidi.+ 2 Kwa maana sisi sote hujikwaa mara nyingi.+ Ikiwa yeyote hajikwai katika neno,+ huyo ni mtu mkamilifu,+ anayeweza kuuongoza kwa lijamu mwili wake wote pia. 3 Tukiweka lijamu+ katika vinywa vya farasi ili watutii,+ sisi huuongoza mwili wao wote pia. 4 Tazameni! Hata mashua, ingawa ni kubwa sana nazo huendeshwa na pepo kali, hizo huongozwa na mtambo wa usukani+ ulio mdogo sana ili kwenda pale ambapo mwelekeo wa mtu aliye kwenye usukani anataka.
5 Hivyo, pia, ulimi ni kiungo kidogo na bado hujigamba kwa njia kubwa.+ Tazameni! Ni moto mdogo tu unaohitajika ili kuuwasha mwitu mkubwa! 6 Basi, ulimi ni moto.+ Ulimi ni ulimwengu wa ukosefu wa uadilifu kati ya viungo vyetu, kwa maana huutia doa mwili+ wote na kuuwasha moto mzunguko wa uhai wa asili nao huwashwa moto na Gehena.* 7 Kwa maana kila aina ya mnyama-mwitu na vilevile ndege na kitu kinachotambaa na kiumbe cha baharini ni vya kufugwa navyo vimefugwa na binadamu.+ 8 Lakini ulimi, hakuna hata mmoja wa wanadamu anayeweza kuufuga. Huo ni kitu kitundu chenye kudhuru, umejaa sumu yenye kuua.+ 9 Kwa huo sisi humbariki Yehova,+ naam, Baba,+ na bado kwa huo sisi huwalaani+ wanadamu ambao wamekuja kuwako “kwa mfano wa Mungu.”+ 10 Kubariki na kulaani hutoka katika kinywa kilekile.
Haifai, ndugu zangu, mambo haya kuendelea kutendeka kwa njia hiyo.+ 11 Je, chemchemi+ hutokeza matamu na machungu kutoka katika shimo lilelile? 12 Ndugu zangu, je, mtini unaweza kuzaa zeituni au mzabibu kuzaa tini?+ Wala maji ya chumvi hayawezi kutokeza maji matamu.
13 Ni nani aliye na hekima na mwenye uelewaji kati yenu? Na aonyeshe kutokana na mwenendo wake mzuri matendo+ yake kwa upole ulio wa hekima. 14 Lakini ikiwa mna wivu+ mkali na ugomvi+ katika mioyo yenu, msiwe mkijigamba+ na kusema uwongo juu ya ile kweli.+ 15 Hii siyo hekima inayoshuka kutoka juu,+ bali ni ya kidunia,+ ya kinyama, ya roho waovu.+ 16 Kwa maana mahali ambapo pana wivu+ na ugomvi, hapo pana machafuko na kila jambo baya.+
17 Lakini hekima+ inayotoka juu kwanza kabisa ni safi kiadili,+ kisha yenye kufanya amani,+ yenye usawaziko,+ tayari kutii, yenye kujaa rehema na matunda mema,+ haifanyi tofauti zenye ubaguzi,+ si ya kinafiki.+ 18 Zaidi ya hayo, mbegu ya tunda+ la uadilifu+ hupandwa chini ya hali zenye amani+ kwa wale wanaofanya amani.+