Yakobo
2 Ndugu zangu, je, mnashika imani ya Bwana wetu Yesu Kristo, utukufu wetu,+ kwa matendo ya kupendelea?+ 2 Kwa maana, mtu aliye na pete za dhahabu kwenye vidole vyake na aliyevaa mavazi ya fahari akiingia katika kusanyiko lenu,+ lakini mtu maskini aliyevaa mavazi yenye uchafu akiingia pia,+ 3 mnamtazama kwa kibali+ yule aliyevaa mavazi ya fahari na kumwambia: “Wewe kalia kiti hiki hapa mahali pazuri,” nanyi mnamwambia yule maskini: “Wewe simama,” au: “Kalia kiti kile pale chini ya kiti changu cha miguu,” 4 ninyi mna tofauti za kitabaka katikati yenu wenyewe+ nanyi mmekuwa waamuzi+ wanaotoa maamuzi maovu,+ sivyo?
5 Sikilizeni, ndugu zangu wapendwa. Mungu alichagua walio maskini+ kwa habari ya ulimwengu ili wawe matajiri+ katika imani na warithi wa ufalme, aliowaahidi wale wanaompenda,+ sivyo? 6 Ingawa hivyo, ninyi mmemvunjia heshima mtu maskini. Matajiri huwakandamiza+ ninyi, nao huwakokota ninyi na kuwapeleka mbele ya mahakama,+ sivyo? 7 Wao hulikufuru+ lile jina zuri ambalo kwa hilo mliitwa,+ sivyo? 8 Basi, mkizoea kufanya sheria ya kifalme+ kulingana na andiko: “Mpende jirani yako kama wewe mwenyewe,”+ mnafanya vema kabisa. 9 Lakini mkiendelea kuonyesha upendeleo,+ mnafanya dhambi, kwa maana sheria+ inawakaripia ninyi kuwa ni wakosaji.
10 Kwa maana yeyote anayeshika Sheria yote lakini ajikwae katika jambo moja, amekosa juu ya zote.+ 11 Kwa maana yeye aliyesema: “Usifanye uzinzi,”+ alisema pia: “Usiue.”+ Basi, ikiwa hufanyi uzinzi lakini unaua, umekosa juu ya sheria. 12 Endeleeni kusema na kutenda kama wale watakaohukumiwa kwa sheria ya watu huru.+ 13 Kwa maana yeye asiye na mazoea ya kuonyesha rehema atapata hukumu yake bila rehema.+ Rehema hufurahi kwa njia ya ushindi juu ya hukumu.
14 Ina faida gani, ndugu zangu, kama mtu fulani akisema ana imani+ lakini hana matendo?+ Je, imani hiyo inaweza kumwokoa?+ 15 Ikiwa ndugu au dada yuko uchi naye hana chakula cha kutosha kwa ajili ya siku,+ 16 na mmoja wenu amwambie: “Nenda kwa amani, jipashe moto na kula vizuri,” lakini ninyi mkose kumpa mahitaji ya mwili wake, ina faida gani?+ 17 Vivyo hivyo, pia, imani, ikiwa haina matendo,+ imekufa yenyewe.
18 Hata hivyo, mtu fulani atasema: “Wewe una imani, nami nina matendo. Nionyeshe imani yako bila matendo, nami nitakuonyesha imani yangu kwa matendo yangu.”+ 19 Wewe unaamini kuna Mungu mmoja, sivyo?+ Unafanya vema kabisa. Hata hivyo roho waovu nao wanaamini na kutetemeka.+ 20 Lakini je, unataka kujua, Ee mwanadamu asiye na akili, kwamba imani bila matendo haizai? 21 Je, Abrahamu baba+ yetu hakutangazwa kuwa mwadilifu kwa matendo baada ya kumtoa Isaka mwana wake juu ya madhabahu?+ 22 Mnaona kwamba imani yake ilitenda pamoja na matendo yake na kwa matendo yake imani yake ilikamilishwa,+ 23 na andiko likatimizwa linalosema: “Abrahamu alikuwa na imani katika Yehova, na ikahesabiwa kwake kuwa ni uadilifu,”+ naye akaitwa “rafiki ya Yehova.”+
24 Mnaona kwamba mtu hutangazwa kuwa mwadilifu+ kwa matendo,+ na si kwa imani peke yake.+ 25 Vivyo hivyo, je, Rahabu+ yule kahaba hakutangazwa pia kuwa mwadilifu kwa matendo, baada ya kuwakaribisha wale wajumbe na kuwatoa nje kwa njia nyingine?+ 26 Kwa kweli, kama vile ambavyo mwili bila roho umekufa,+ vivyo hivyo pia imani bila matendo imekufa.+