Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g93 7/22 kur. 4-5
  • Watu Wadogo, Mikazo Mikubwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Watu Wadogo, Mikazo Mikubwa
  • Amkeni!—1993
  • Habari Zinazolingana
  • Kulea Watoto tangu Uchanga
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • Zoeza Mtoto Wako Tangu Utoto Mchanga Sana
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Mzazi Mmoja, Matatizo Mengi
    Amkeni!—2002
  • Funguo za Elimu Nzuri
    Amkeni!—1995
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1993
g93 7/22 kur. 4-5

Watu Wadogo, Mikazo Mikubwa

“Kwa hakika, huzuni za watoto ni ndogo, lakini watoto ni wadogo pia.” —Percy Bysshe Shelley.

TAZAMA mchoro ulio hapo chini wa kofia ndefu ya duara. Kwa kuitazama mara moja kofia hiyo yaonekana kuwa ndefu kuliko ukingo uonekanavyo mpana. Hata hivyo, kwa uhalisi, urefu na upana ni sawa. Vipimo vyaweza kuamuliwa vibaya kwa urahisi.

Ndivyo ilivyo rahisi kwa watu wazima kuamua vibaya viwango vya mkazo wa akili wa mtoto. ‘Matatizo ya watoto ni madogo sana,’ wengine hufikiri. Lakini kufikiri huko ni kwa madanganyo. “Watu wazima hawapaswi kuamua matatizo kwa kadiri yayo,” chaonya kitabu Childstress!, “lakini kwa kadiri ya maumivu yanayotokeza.”

Katika visa vingi kiwango cha maumivu ya watoto kiko juu zaidi ya vile watu wazima wanajua. Hilo lilithibitishwa na uchunguzi mmoja ambapo wazazi waliulizwa wakadirie hali ya hisia-moyo ya watoto wao. Karibu wote walijibu kwamba watoto wao walikuwa na “furaha sana.” Hata hivyo, watoto walipoulizwa wakiwa mbali na wazazi wao, wengi wa hao walijieleza kuwa “wasio na furaha” na hata “wenye taabu.” Watoto hukabili hofu ambazo wazazi huziona kuwa ndogo sana.

Katika uchunguzi mwingine, ulioongozwa na Dakt. Kaoru Yamamoto, kikundi cha watoto kiliambiwa kiweke matukio 20 ya maisha katika mizani ya mkazo wa akili ya pointi saba. Kisha kikundi cha watu wazima kikaweka matukio hayohayo kulingana na jinsi walivyohisi mtoto angeyaweka. Watu wazima walikosea kwa vitu 16 kati ya 20! “Sote tunafikiri tunajua watoto wetu,” amalizia Dakt. Yamamoto, “lakini kwa kweli mara nyingi zaidi hatuoni au kusikia, wala kuelewa jambo linalowasumbua.”

Wazazi wanapaswa kujifunza maono ya maisha kwa mtazamo mpya: kupitia macho ya mtoto. (Ona sanduku.) Hilo hasa ni jambo la maana sana leo. Biblia ilitabiri kwamba “katika siku za mwisho kutakuwako nyakati zenye mikazo mingi . . . ngumu kushughulika nazo na ngumu kuvumilia.” (2 Timotheo 3:1, The Amplified Bible) Watoto pia wanapatwa na mkazo kama huo; mara nyingi wao ndio hupatwa nao sana. Ijapokuwa baadhi ya mikazo ya watoto huwa ni ya “ujanani,” mingine huwa si ya kawaida na hustahili uangalifu wa pekee.—2 Timotheo 2:22.

[Sanduku katika ukurasa wa 5]

Kupitia Macho ya Mtoto

Kifo cha Mzazi = Hatia. Kukumbuka mawazo ya mara kwa mara ya hasira kuelekea mzazi, mtoto anaweza kuwa na hisia zilizofichika za kuhusika na kifo cha mzazi.

Talaka = Kuachwa. Akili ya mtoto husema kwamba ikiwa wazazi wanaweza kuacha kupendana, wanaweza pia kuacha kumpenda.

Ulevi = Mkazo. Claudia Black aandika: “Mazingira ya kila siku ya woga, kuachwa, kukanwa, kutopatana, na jeuri halisi au inayoweza kutoka katika nyumba yenye ulevi si mazingira yanayofaa yenye afya.”

Mapigano ya Wazazi = Woga. Uchunguzi wa wanafunzi 24 ulionyesha kuwa mapigano ya wazazi hutokeza mkazo wa akili sana hivi kwamba yanatokeza mfululizo wa kutapika, mtetemo wa uso, kupoteza nywele, kupoteza au kuongeza uzani, na hata vidonda vya tumbo.

Matimizo Zaidi = Mvurugo. “Mahali popote watoto waendapo” akaandika Mary Susan Miller, “wanaonekana wamo kwenye mashindano makali ambayo wamepangiwa na watu wazima.” Wakisongwa kuwa wanafunzi bora zaidi shuleni, nyumbani, na hata michezoni, mtoto huyo hapati kushinda kamwe, na mbio hiyo haiishi kamwe.

Mtoto Mwingine Aliyezaliwa = Hasara. Sasa kushiriki na mwingine upendo na uangalifu wa mzazi, huenda mtoto akahisi kwamba amepoteza mzazi badala ya kupata ndugu au dada.

Shule = Hangaiko la Kutengana. Kwa Amy, kumwacha mama yake na kwenda shuleni kulikuwa kunaumiza sana na kushusha moyo.

Makosa = Kushuswa. Wakiwa na udhaifu wa kujifikiria, watoto “huelekea kuona mambo kuwa matatizo mazito sana kuliko yalivyo hasa,” asema Dakt. Ann Epstein. Alipata kwamba kushushwa kulikuwa mojapo sababu za kawaida sana za mtoto kujiua.

Ulemavu = Mvurugo. Kando na dhihaka za marika wasio na huruma, mtoto mwenye ulemavu wa kimwili au kiakili huenda akahitaji kuvumilia ukosefu wa subira wa walimu na washiriki wa familia ambao humtamausha kwa ajili ya kutotimiza mambo yenye kupita uwezo wake.

[Picha katika ukurasa wa 4]

Kofia ndefu ya duara ya kikale

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki