Je! Mungu Anajali?
Kwa nini yeye aruhusu kuteseka?
Je! Kutakwisha Wakati Wowote?
Hayo ni maswali ya kushangaza, sivyo? Yanatokea katika jalada la broshua iliyotangazwa na Mashahidi wa Yehova. Je! umeisoma? Tayari imewapatia watu wengi faraja na tumaini. Mwanamke mmoja kutoka Philadelphia, Pennsylvania, U.S.A., aandika hivi kuhusu broshua hiyo:
“Sikujua kama ingewezekana kutunga maneno pamoja kwa uzuri sana na kwa njia yenye kuchangamsha moyo. Ni kana kwamba nilikuwa katika chumba chenye giza na kwa ghafula mtu akawasha taa; Nikatambua hivi: ‘Mungu anajali kweli!’
“Sikuzote nimekuwa mtu mwenye kutegemea sayansi. Kwa hiyo, hotuba, makala, au sinema zinazoegemea sayansi zimenipa nguvu zaidi iwapo nimevunjika moyo. Hata hivyo, broshua hii imenipa nguvu tena na hata zaidi imenigusa kwa njia nyororo na yenye upendo.
“Jambo la kwanza linalokuvutia ni jalada. Inavutia kwa sababu hao ni watu halisi. Sura ya kila mmoja wao inaonyesha hangaiko la swali lililoandikwa kwa chapa nzito nyeusi, ‘Je! Kweli Mungu Anatujali?’ Watu hao wana sura zinazoonyesha jinsi kila mtu anavyohisi siku hizi.
“Habari iliyomo inaeleweka kwa urahisi. Ni sahili, na yenye kufaa, na ni yenye maana. Inatoa sababu. Inafurahisha sana na ni rahisi sana kusoma hivi kwamba mara unapoanza kuisoma, huwezi kuiweka chini.”
Ikiwa ungependa habari zaidi, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au kwa anwani yoyote ifaayo iliyoorodheshwa katika ukurasa wa 5.
[Picha katika ukurasa wa 32]
JE! KWELI MUNGU ANATUJLI/
Ikiwa ndivyo, kwa nini yeye aruhusu kuteseka?
Je! Kutakwisha wakati wowote?