Tukio Usilopaswa Kukosa
“Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.” Maneno hayo ya Bwana wetu Yesu Kristo, yapatikanayo kwenye Luka 22:19, yalisemwa wakati alipoanzisha Ukumbusho wa kifo chake. Kifo cha Yesu ndicho kilichofungulia wanadamu tazamio la kupata uhai wa milele katika hali za Paradiso. Kwa hiyo kifo chake ni kitu tupaswacho kukumbuka.
Je! wewe utaadhimisha Ukumbusho wa kifo hicho mwaka huu?
Tafadhali pokea mwaliko huu kutoka kwa Mashahidi wa Yehova ili ukutane pamoja nao katika kufanya ukumbusho wa tukio hilo la maana. Mwadhimisho huo utakuwa baada ya jua kushuka katika tarehe ilinganayo na Nisani 14 katika kalenda-mwezi ya Biblia. Mwaka huu tarehe hiyo ni Jumamosi, Machi 26. Mashahidi wa Yehova wa kwenu waweza kukuambia mahali na wakati hususa ambapo tukio hili litaadhimishwa katika jumuiya yenu.