“Shukrani”
Hilo ndilo mwanafunzi kijana katika Japani alitaka kuwasilisha. Msichana huyo alieleza kwamba alikuwa amepokea zawadi maalumu shuleni za insha alizoandika kwa kutumia makala za Amkeni! alizosoma.
“Kabla ya kuziandika,” yeye akaongezea, “nilikuwa nikiyaweka magazeti nyumbani bila kuyasoma. Nilipofikiria jinsi hayo magazeti yamekuwa yenye faida kwangu, nilijisemea, ‘Haya ndiyo magazeti ambayo nimekuwa siyasomi.’ Hisia za msikitiko zilinikumba. Tangu wakati huo, nimekuwa nikiyasoma hayo magazeti kama nipasavyo.”
Kwa kuthamini, mwanafunzi huyu aliandika zaidi hivi: “Hayo magazeti ni yenye manufaa sana kwa kunisaidia kushughulikia majaribu yote mbalimbali ninayokabili shuleni. Asanteni kwa kuandaa sikuzote makala nzuri sana hivyo. Nitaendelea kutazamia kuyapokea.”
Kwa ukawaida Amkeni! hutokeza makala ambazo husaidia vijana kukabili matatizo wayakabiliyo nyumbani na shuleni. Ikiwa ungependa nakala ya Amkeni! au ungependa mtu akutembelee nyumbani ili akusaidie kupata majibu yenye kutegemea Biblia ya matatizo ambayo huenda ukawa nayo, tafadhali andikia I.B.S.A., Box, 47788, Nairobi, Kenya, au anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa 5.