Mataifa Adui Yaliyoshambulia Israeli
KUZUNGUKA Israeli yalikuwa mataifa adui ambayo yalikuwa na nia ya kuchukua urithi walo. Je, Israeli lingeshindwa? Mradi Israeli lilibaki likiwa lenye uaminifu, uamuzi ulikuwa upande walo. “BWANA alipiga vita kwa ajili ya Israeli.”—Yoshua 10:14.
Hili lilionyeshwa waziwazi wakati wa utawala wa Mfalme Yehoshafati (936-c. 911 K.W.K.). Majeshi yaliyoungana ya Amoni, Moabu, na Mlima Seiri yalikuja dhidi ya Yuda. Yehoshafati akamsihi Yehova hivi: ‘Tazama jinsi wanavyokuja kututupa kutoka milki yako, uliyoturithisha. Ee Mungu wetu je! hutawahukumu?’ Bila shaka Yeye angefanya hivyo! Yuda lilihakikishiwa hivi: “Vita si yenu bali ni ya Mungu.” Yehova aliwatatanisha adui, akiwafanya wachinjane.—2 Mambo ya Nyakati 20:1-23.
Mwishowe, baada ya karne nyingi za kupigania Israeli, Yehova aliruhusu mataifa adui yalishinde. Katika 740 K.W.K. Waasiria walimaliza ufalme wa makabila kumi “kwa sababu wana wa Israeli walikuwa wametenda dhambi juu ya BWANA.” (2 Wafalme 17:7-18) Kisha katika 607 K.W.K., kwa sababu ya kutotii kwao ufalme wa makabila mawili uliharibiwa na Wababiloni. (2 Wafalme 21:10-15; 22:16, 17) Kipindi hiki cha historia ya Israeli chakazia umaana wa kumtii Yehova.