Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g96 11/8 kur. 3-4
  • Je, Dini za Ulimwengu Zakaribia Mwisho Wazo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Dini za Ulimwengu Zakaribia Mwisho Wazo?
  • Amkeni!—1996
  • Habari Zinazolingana
  • Nani Anayependezwa na Dini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Kwa Nini Kupendezwa na Dini Nyingine?
    Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu
  • Je! Dini Yoyote Ni Nzuri vya Kutosha?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Jinsi Dini za Uwongo Zinavyopotosha Ukweli Kumhusu Mungu
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1996
g96 11/8 kur. 3-4

Je, Dini za Ulimwengu Zakaribia Mwisho Wazo?

NA MLETA-HABARI WA AMKENI! KATIKA SWEDEN

JE, KICHWA hiki chafanya ujiulize: ‘Inawezekanaje? Je, si dini za ulimwengu zina nguvu sana na ni zenye uvutano kotekote duniani leo?’

Ndiyo, zijapopitia matatizo mengi, hizo zaonekana kuwa zenye nguvu nyingi na zenye uvutano. Katika karne hii ya 20, dini imetiliwa shaka na kufichuliwa kuliko wakati mwingine wowote katika historia ya wanadamu. Waastronomia wamechunguza ulimwengu wote mzima kwa darubini-upeo zilizo kubwa sana, na wasafiri wa anga ya nje wamevuka-vuka anga; na kama alivyosema Msovieti mmoja ambaye ni msafiri wa anga ya nje, wao hawajaona “Mungu wala malaika.” Wanafizikia wamepasua mata katika vipande vidogo-vidogo zaidi bila kugundua jambo lolote lile linalodokeza kwamba uhai ulianza kwa njia ya kimungu. Wanabiolojia na wataalamu wa maisha ya zamani wadai kwamba wameunganisha tena mnyororo mrefu wa mageuzi, tokea amiba hadi mwanadamu, bila kupata jambo lolote linalodokeza uumbaji mahali popote pale katika mnyororo huo.

Hata hivyo, hekima ya kilimwengu na falsafa ya kufuatia vitu vya kimwili zimeshindwa kuondosha mtazamo wa kidini duniani, na mamlaka za kiatheisti na falsafa hazijafanikiwa pia. Kwa zaidi ya miaka 70, Ukomunisti wenye kutawala kiimla na wa kiatheisti ulisema kwamba dini ni ushirikina na “kasumba ya watu,” ukawanyang’anya viongozi wa kidini vyeo vyao na kupiga marufuku utendaji wao, ukaharibu au kupora makanisa na mahekalu, na kupotosha na kuua kimakusudi waabudu. Lakini matendo hayo hayakuondoa mtazamo wa kidini. Mara tu baada ya serikali hizo kuanguka, dini iliinuka tena kana kwamba imepata nguvu mpya. Katika mabara ambayo zamani yalikuwa ya Kikomunisti, watu tena wanarudia mahekalu yao ya zamani, wakipiga magoti katika ibada yao yenye uchaji kama wazazi wao wa kale walivyofanya kabla yao.

Mtazamo wa kidini ungali wawaka katika sehemu fulani za ulimwengu. Kila mwaka jiji la Mecca, katika Saudi Arabia, hupokea mamilioni ya wahiji Waislamu kutoka kotekote duniani. St. Peter’s Square katika Vatikani mara nyingi hujaa kupita kiasi kwa waamini Wakatoliki wanaotaka kumwona papa na kutumaini kupata baraka yake. Mamilioni ya waumini Wahindu huendelea kumiminikia mamia ya sehemu zao takatifu ambazo ziko kando-kando ya mito “mitakatifu” katika India. Wayahudi wachaji humiminikia ule Wailing Wall katika Yerusalemu ili kusali na kuacha sala zao zilizoandikwa kwenye mianya ya ukuta.

Ndiyo, yaonekana kuwa haiwezekani kuondoa dini kutoka kwa wanadamu. “Mwanadamu kulingana na maumbile yake ni kiumbe cha kidini,” akasema mkuu wa serikali aliyezaliwa Ireland Edmund Burke. Kitarakimu, watu 5 kati ya kila watu 6 duniani wanajihusisha kwa njia moja au nyingine na dini fulani. Kulingana na tarakimu za hivi majuzi, kuna wafuasi wapatao bilioni 4.9 wa dini mashuhuri ulimwenguni, huku kukiwa na watu wapatao milioni 842 pekee ambao si wa kidini.a

Kwa maoni haya, je, inafaa kuamini kwamba dini za ulimwengu zinakaribia mwisho wazo? Na ikiwa ndivyo, mwisho wazo utakuja lini na kwa njia gani? Je, kuna dini yoyote itakayobaki? Ebu tuzungumzie maswali haya katika makala mbili zifuatazo.

[Maelezo ya Chini]

a “Watu wasio wa kidini” watia ndani: “Watu wanaodai kuwa wao si wafuasi wa dini, si waamini, waagnosti, wenye kukana mambo ya kidini, na watu wa kilimwengu ambao hawana dini na ni wenye ubaridi kuelekea dini zote.”

[Picha katika ukurasa wa 3]

St. Peter’s Square, Vatican City

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki