Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w78 8/1 kur. 3-5
  • Nani Anayependezwa na Dini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Nani Anayependezwa na Dini?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • JE! WENGI WANAPENDEZWA?
  • MAELEKEO YA KIDINI YA KUTIA BIDII MPYA YAPINGWA NA MWENENDO MPOTOVU
  • MAANA YA HAYO NI NINI?
  • Je! Dini Yoyote Ni Nzuri vya Kutosha?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Ninaweza Kuipataje Dini ya Kweli?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Kuzoea Dini Safi Kwa Ajili Ya Kuokolewa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Sehemu ya 24: Sasa na milele—Mazuri ya Milele ya Dini ya Kweli
    Amkeni!—1990
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
w78 8/1 kur. 3-5

Nani Anayependezwa na Dini?

Ndiyo Hapana

Je! una dini? □ □

Je! unapendezwa na dini? □ □

Inaelekea uliweka alama ya “Ndiyo” katika ulizo la kwanza. Watu wengi wangefanya hivyo, kwa maana watu zaidi ya bilioni mbili na nusu ni washiriki wa dini kubwa za ulimwengu. Mamilioni wengine wanashirikiana na dini nyingine au wana imani za kidini.

Namna gani jambo hilo la pili: Je! unapendezwa na dini? Je! unaona kutaka sana kujua dini ya kweli ni sehemu ya maana ya maisha yako?

Watu wengi leo hawapendezwi sana na dini. Wala hawazungumzi sana habari za dini wala hawaruhusu dini igeuze maisha zao. Namna gani wewe mwenyewe? Namna gani ikiwa tungechunguza jirani zako, wafanya kazi au wanashule wenzako, tukiwauliza kama wanakuona unapendezwa na dini, unadhani wengi wao wangejibuje?

JE! WENGI WANAPENDEZWA?

Kwa kuchunguza mambo fulani, labda utafahamu sababu gani ni vigumu kulijibu ulizo hili ‘Nani anayependezwa na dini?’

Kwa upande mwingine, kuna ushuhuda unaoonyesha kwamba watu wengi wanapendezwa na dini leo. Kwa mfano, umepata kuangalia kwamba kuna vitabu vingi na makala nyingi za magazeti zinazozungumza habari za dini? Mwandikaji mmoja alieleza hivi juu ya vitabu vya dini vinavyouzwa:

“Wauzaji walikuwa wakiuzia watu wa dini vitabu vya dini nao hawakuweka dukani kitabu kilichodharau dini isipokuwa ingekuwa dini ya ‘wasio Wakristo,’ ambayo kila mtu alijua kwamba haikuwa dini ya kweli bali ni ibada ya sanamu na mambo ya upagani. Lakini sasa wauzaji wanauzia vilevile watu wasiokwenda kanisani vitabu vya dini kwa wingi, watu wanaotaka kujua namna watu wa dini wanavyokuwa, na desturi hiyo, na kama wao vilevile wangefurahia zaidi kuwa hivyo.”

Tena, bila shaka umepata kuona ushuhuda mwingine unaoonyesha namna watu wengi wanavyopendezwa na dini: Watu wanapigana, ndiyo, hata kuuana kwa sababu ya dini. Ni kweli kwamba labda hujapata kufikiria hivyo, lakini ndivyo ilivyo.

Kwa mfano, namna gani mapigano makali yanayofanyika kati ya madhehebu ya kidini huko Filipino au Lebanoni? Je! wayakumbuka mapigano ya Wakatoliki na wafuasi wa dini ya Buddha yaliyotokea huko Vietnam? Wala hatuwezi kukosa kuangalia ukatili wa huko Ireland kati ya Wakatoliki na Waprotestanti​—⁠ambako watu wanapigwa risasi au kupasuliwa vipande vipande na makombora kwa sababu ya dini yao. Taarifa ya karibuni iliyotolewa na Associated Press ilianza hivi:

“Dini za ulimwengu zinafundisha amani, haki na upendo, hata hivyo zinatokeza hali ya kujipa wajibu, kuonyesha ushikamanifu, shauku nyingi mno na mara nyingine vita. . . . ‘Bado vita vibaya sana na vya kumwaga damu vinapiganwa katika jina la Mungu.’”

Kupigana katika jina la dini kunaweza kuonyesha kwamba watu wengi wanapendezwa sana na dini. Walakini, je! wewe wadhani kwamba ndivyo walivyo wafanya kazi wenzako, wanashule wenzako au watu wengi katika mtaa wako? Je! wanaweza kukuambia kwa ukweli mambo ambayo dini yao inafundisha na sababu yake?

Kwa mfano, katika mwaka 1977 mwalimu wa filosofia Walter Kaufmann aliandika habari za imani ya kidini katika nchi moja. Tunapokuambia alivyosema, hatutataja jina la nchi na maandishi matakatifu aliyotaja. Jaribu uone kama anayosema yangekuwa hivyo ikiwa ungejaza jina la nchi yako na maandishi ya kidini yanayokubaliwa na watu wengi huko:

“Watu wengi katika [nchi yako] hawajui sawasawa mambo wanayoamini, hawajalifikiria sana jambo hilo. Wakiulizwa pasipo kutazamia juu ya imani yao, majibu yao yanategemea wakati ule walipozungumza maulizo hayo mara ya mwisho miaka mingi iliyopita. Kwa kawaida watu wanaosema kwamba wanaamini maelezo ya [maandishi yao matakatifu] hawajui yaliyo [katika maandishi hayo], nao wangeshangaa sana ikiwa mtu angewaambia.”

Ndiyo, kwa upande mmoja dini inaonekana ‘ikitokeza hali ya kujipa wajibu, kuonyesha ushikamanifu, shauku nyingi mno na mara nyingine vita’ na, upande mwingine, watu wengi hawajui mambo ambayo dini yao inafundisha, wala hawataki kuchunguza.​—⁠Linganisha Warumi 10:2.

Ebu angalia yaliyosemwa na makala hii ya gazeti:

MAELEKEO YA KIDINI YA KUTIA BIDII MPYA YAPINGWA NA MWENENDO MPOTOVU

Je! ungekubali kwamba hilo linaonyesha sawasawa hali unayoiona katika mtaa wako? Kama uchunguzi mmoja wa taifa lote uliofanywa katika United States ulivyoonyesha: “Dini inazidi kuvuta watu, lakini mwenendo mwema unaendelea kukosa nguvu. Walimwengu wangetoa ushuhuda mwingi unaoonyesha kwamba dini haigeuzi sana maisha zetu.”

Wala hutaona jambo hilo kuwa la nchi moja tu. Watu katika kila nchi wanakubali kwamba wao ni wanadini lakini maisha zao zinaonyesha kwamba dini haiwageuzi sana.

Taarifa moja kutoka Canada inafahamisha sababu moja. Ilisema habari ya watu walio na njaa ya kiroho, lakini ikasema kwamba dini nyingi zinaleta “magumu, mengi ya kidini yenye kuenea pote,” mahali pa kuwashibisha. Mtazamaji mmoja katika mkutano wa Canada wa maaskofu wa Kikatoliki alilalamika akisema kwamba, watu wengi wanajibu hivi:

“Kila mtu leo ana maulizo mengi moyoni mwake. Kanisa haliwezi kukupa majibu juu ya dini. Ijapokuwa nina imani, kuna kasoro fulani katika kanisa.”

Au umepata kusikia maneno kama haya yaliyosemwa na mwanamume mmoja aliyependa sana kutembelea mahali fulani akiwa amepanda baisikeli badala ya kwenda kwenye ibada za dini: “Wahubiri wengi wanahubiri ili wapate fedha. Siku hizi kazi ya kuhubiri imekuwa biashara kubwa.”

MAANA YA HAYO NI NINI?

Yote hayo yana maana gani kwako na jamaa yako?

Ni kweli kwamba leo shauku nyingi mno ya kidini inaweza kuongoza watu kwenye chuki, uuaji na vita. Hata hivyo pamoja na hayo kuna ushuhuda unaoonyesha kwamba watu wengi hawaridhiki na dini. Wengi wanaona njaa ya kiroho au wanataka sana kuabudu lakini wanavurugwa akili nao hawajui sana habari za dini. Labda wanaona haya kuwa mtu wa dini au labda wanaona kwamba dini inawavuruga sana akili. Je! ndivyo wewe unavyoona?

Au, labda hujioni mwenyewe kuwa mtu wa dini sana. Labda unapendezwa na dini yako, ukisadiki kwamba ni ya kweli. Kwa vyo vyote, kuna sababu nzuri ya kukubali mwito wa kufikiria dini ya kweli. Kitabu kinachoitwa The Great Religious Leaders kilisema hivi: “Tukijua namna dini inavyompa mtu faida, na namna nguvu za mtu zinavyoongezeka kwa kufahamu sawasawa na kwa kuwa na dini, maisha yanapaswa yaendelee kuwa yenye kufaa zaidi sana.”

Dini ya kweli haipaswi kufanya ‘maisha yawe yenye kufaa zaidi sana’ tu, bali twaweza kukuhakikishia kwamba mambo ya hakika yanaonyesha inafanya hivyo! Lakini kabla hujakubaliana wala kutokubaliana na maneno hayo, tunakukaribisha uifikirie zaidi habari ya dini ya kweli. Je! kuna dini moja ya kweli tu? Ikiwa ndivyo, ungeweza kuitambuaje? Nayo yaweza kuwa na maana gani kwako?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki