Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g90 12/8 kur. 18-25
  • Sehemu ya 24: Sasa na milele—Mazuri ya Milele ya Dini ya Kweli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sehemu ya 24: Sasa na milele—Mazuri ya Milele ya Dini ya Kweli
  • Amkeni!—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mazuri Gani?
  • Kuyajazia Mapengo
  • Uvutio Hautoshi
  • Kujiweka Huru Na Dini Bandia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Kuzoea Dini Safi Kwa Ajili Ya Kuokolewa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Ninaweza Kuipataje Dini ya Kweli?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Nani Anayependezwa na Dini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1990
g90 12/8 kur. 18-25

Wakati Ujao wa Dini kwa Kutegemea Wakati Wayo Uliopita

Sehemu ya 24: Sasa na milele—Mazuri ya Milele ya Dini ya Kweli

“Dini, ikiwa imepambwa kweli za kimbingu, huhitaji kuonwa tu ili ivutie.”—William Cowper, mshairi Mwingereza wa karne ya 18

HAKUNA cha kuvutia kuhusu dini bandia. Imepitisha aina ya kibinadamu katika karne 60 za shida na mateso. Uwongo wayo, udanganyifu, hila, na njia zenye chuki zimeipa sura mbaya machoni pa Mungu na pa binadamu pia. Kando kabisa na kupambwa kwa kweli za kimbingu, dini bandia ni kinyume cha ukweli na uzuri.

Karibuni majeshi ya Mungu ya kuchinja yataimwaga dini bandia kama takataka iingie katika shimo la mtokomeo wa milele. Muda mfupi baada ya hapo, sehemu nyingine yote ya mfumo wa Shetani itafuata. Lakini dini ya kweli, vilevile wale waizoeao, itaendelea kuishi. Itakuwa shangwe kama nini wakati huo kuona mazuri yayo ya milele yakionyeshwa kwa kadiri ambayo sisi leo twaweza kuwazia kwa uhaba tu!

Mazuri Gani?

Ni mengi mazuri ya dini ya kweli. Hapa pana machache tu. Kwa nini usichukue wakati wa kutazama maandiko ya Biblia yaliyoonyeshwa bila manukuu ambayo yathibitisha kwamba mazuri haya ya milele yana msingi wa Biblia?

Miongoni mwa mazuri mengi ya milele ya dini ya kweli mna haya:

◼ Yategemea ukweli wa Mungu asiyekosea, ambaye jina lake ni Yehova, ambaye sisi twaweza kumtegemea bila masharti.—Zaburi 83:18; Isaya 55:10, 11.

◼ Yaweza kupatwa na kila mtu mwenye moyo mnyenyekevu, wala haikuwekwa akiba kwa ajili ya wakuu au wenye uelewevu mwingi peke yao.—Mathayo 11:25; 1 Wakorintho 1:26-28.

◼ Haijali rangi ya mtu, cheo cha kijamii, na msimamo wa kiuchumi.—Matendo 10:34, 35; 17:24-27.

◼ Hutoa tumaini lenye msingi imara la uhai katika ulimwengu wenye amani na usalama bila majonzi, magonjwa, shida, na kifo.—Isaya 32:18; Ufunuo 21:3, 4.

◼ Huandaa mwundo ambamo washiriki wayo waweza kuishi wakiwa udugu wenye uaminifu-mshikamanifu ulimwenguni pote, wakiwa wameungamana katika fundisho, mwenendo, na roho.—Zaburi 133:1; Yohana 13:35.

◼ Hutolea kila mtu—mwanamume, mwanamke, na mtoto—fursa ya kushiriki kwa utendaji katika kazi ya Mungu, kujaza kusudi katika maisha.—1 Wakorintho 15:58; Waebrania 13:15, 16.

◼ Hutuonya juu ya hatari zilizofichika, ikituagiza jinsi ya kujiendesha kwa njia ya kupata manufaa.—Mithali 4:10-13; Isaya 48:17, 18.

Na kwa nini yaweza kusemwa kwamba mazuri haya ni ya milele? Kwa sababu tu yatadumu muda mrefu kama dini ya kweli yenyewe—milele.

Kuyajazia Mapengo

Yaweza kusemwa kwamba kifo ni mmoja wa maadui wakubwa zaidi wa ukweli, kwa kuwa mara nyingi watu hutimuka kwenda kwenye makaburi yao wakiwa na habari ambazo hakuna wanadamu wengine wowote wazijuao. Maelezo juu ya ilivyokuwa hasa kuhusu hata matukio ya juzijuzi tu—kwa kielelezo, kuuawa kwa rais wa United States J. F. Kennedy katika 1963—yangali jambo la kubishaniwa. Mambo ya uhakika ni nini? Nani hasa ajuaye? Wengi ambao wangeweza kujua hawako hai tena. Na ikiwa hivyo ndivyo ilivyo kuhusu tukio la miaka 26 tu iliyopita, namna gani matukio yaliyotendeka mamia au hata maelfu ya miaka iliyopita?

Kwa kuongezea, wanahistoria ni wanadamu tu, wenye mipaka ya kujua mambo na ambao hufanya kazi chini ya hali za kibinafsi za kutokamilika na uwezekano wa kufuata maoni ya ubaguzi. Ndiyo sababu mtu mwenye kutazama mambo kama yalivyo hasa apaswa kujiepusha kukazana kwa ushupavu juu ya mambo ambayo yeye hana rekodi yenye mamlaka, iliyovuviwa kimungu kuyahusu.

Kuandika juu ya historia ya kidini hutokeza matatizo kama hayo, kwa kuwa mara nyingi wakuu hawaafikiani juu ya mambo ya uhakika. Katika ule mfululizo “Wakati Ujao wa Dini kwa Kutegemea Wakati Wayo Uliopita,” Amkeni! limejaribu kutokeza mambo ya uhakika yaliyo na uthibitisho wa kutosha, lakini ni lazima ikiriwe kwamba kwa sasa kuna mambo fulani tusiyoyajua hata kidogo. Kwa kielelezo, vikundi vyenye kudai kuwa vya Kikristo vilivyokuwako wakati na baada ya zile Enzi za Giza viliambatana na Ukristo wa kweli kwa kadiri gani?

Juu ya vikundi hivi, profesa wa historia ya kanisa A. M. Renwick aandika hivi: “Utafiti mwingi wa kihistoria ungali wahitajiwa ili kuitokeza hadithi ya kweli na maoni ya kitheolojia ya vikundi hivyo vingi sana.” Kulingana na Renwick, “wakati uliopita wanahistoria wametegemea mno taarifa za maadui wa vikundi vyenye upinzani ili kukadiria fundisho na maadili yavyo.” Bila shaka, kutegemea mno taarifa za marafiki zao huenda pia kukatokeza maoni kombo. Hivyo basi hata baada ya utafiti mwingi wa kihistoria, maswali mengi yangeweza bado kubaki bila kujibiwa.

Namna gani Biblia? Ikiwa kitabu kilichovuviwa kimungu chenye historia fulani ya kidini, yategemeka katika kila jambo isemalo. Lakini husema machache sana juu ya namna zote tofauti-tofauti za dini bandia ambazo zimepata kuwako. Yaeleweka kwamba ingefanya hivyo, kwa kuwa iliandaliwa ili itumike kuwa kitabu cha masomo kwa ajili ya dini ya kweli, si kwa ajili ya iliyo bandia.

Hata kuhusu dini ya kweli, Biblia haituambii kila jambo. Hutuandalia habari za kutosha za kuitambua dini ya kweli kwa mafanikio, lakini nyakati fulani huacha nje maelezo madogo-madogo. Ingawa huenda likawa jambo la kusisimua na la kupendeza kujua maelezo hayo madogo-madogo, kwa sasa si ya muhimu.

Halafu, pia, Biblia ina mapengo ya wakati. Kwa kielelezo, haisemi lililotukia wakati wa ile miaka zaidi ya 400 iliyopita kati ya kumalizwa kwa Maandiko ya Kiebrania, ambayo kwa kawaida huitwa Agano la Kale, na kutokea kwa Yesu. Na tangu Biblia imalizwe, karibu miaka 1,900 imepita.

Hivyo basi kwa sehemu kubwa ya karne 18, hatuna rekodi yoyote iliyovuviwa juu ya Ukristo. Hiyo ndiyo husababisha kutokuwa na uhakika juu ya watu fulani wajidaio kuwa Wakristo, kama ilivyotajwa na mtungaji Renwick. Hata hivyo, yaonekana wazi kwamba angalau watu fulani mmoja mmoja muda wote wa kuteremkia karne hizo walikuwa wakiambatana na Ukristo wa mapema. Hata hivyo, kuna maswali ambayo hayajatatuliwa kuhusu matilaba na uwezekano wa unyofu wa watu fulani mmoja mmoja wa miaka iliyopita. Namna gani juu ya viongozi wa ule Mrekebisho? Hivyo basi, namna gani watu kama Konfyushasi na Muhammadi? Ingawa mifumo ya kisasa ya kidini yaweza kuhukumiwa kisahihi kwa msingi wa matunda yayo, watu mmoja mmoja—hasa ikiwa wamekufa tangu muda mrefu uliopita—mara nyingi hawawezi kuhukumiwa hivyo.

Hata hivyo, ikiwa katika ulimwengu mpya wa Mungu yatakuwa mapenzi ya Muumba kuandikisha upya vitabu vya historia—kutia na vile vya historia ya kidini—itawezekana. Hiyo ni kwa sababu ya uzuri mwingine wa dini ya kweli—uhakikishio wa kwamba wafu watafufuliwa.—Yohana 5:28, 29; Matendo 24:15.

Wazia shangwe ya kupata majibu sahihi kwa maswali yetu kwa kuongea na wanadamu wafufuliwa waliofanya hasa mambo ambayo tumesoma katika vitabu vya historia. Wazia kuweza kujazia maelezo madogo-madogo yaliyokosekana, kama jina la Farao aliyekufa kwenye Bahari Nyekundu na kupatwa na tauni za Misri.

Ikiwa siku fulani rekodi hiyo itaandikwa, itaandikwa ili kumtukuza na kumtetea milele mwanzilishi wa dini ya kweli, Yehova Mungu. Hakuwezi kuwa na shaka juu ya hilo. Hata hivyo, swali ambalo labaki ni hili: Je! wewe utakuwako uisome?

Uvutio Hautoshi

Mazuri ya milele ya dini ya kweli hayaonwi kwa urahisi sikuzote kama vile maneno ya Cowper, yaliyonukuliwa mwanzoni mwa makala hii, yangeelekea kuonyesha. Kwa hiyo, toleo la kwanza la Zion’s Watch Tower and Herald of Christ’s Presence lilitoa maoni yanayofuata miaka 110 iliyopita: “Ukweli, kama ua dogo lenye kiasi katika jangwa la maisha, wazungukwa na karibu kusongwa pumzi na usitawi mwingi wa magugu ya makosa. Ili uupate ni lazima uwe macho wakati wote. Ili uuone uzuri wayo ni lazima ufagilie kando magugu ya makosa na michongoma ya ushupavu. Ili uupate ni lazima uiname kuuchukua.”

Yatumainiwa kwamba habari hizi za “Wakati Ujao wa Dini kwa Kutegemea Wakati Wayo Uliopita” zimesaidia wasomaji wetu ‘kufagilia kando magugu ya makosa na michongoma ya ushupavu’ ili kuyathamini kikamili zaidi mazuri ya milele ya dini ya kweli.

Lakini uthamini hautoshi. Mithali hii ya Kichina ina uelekevu: “Fundisho liingialo masikioni lakini si moyoni ni kama mlo mkuu uliwao katika ndoto.” Ili tunufaike kibinafsi kutokana na mazuri ya milele ya dini ya kweli—si kuota tu juu yayo—ni muhimu kwamba tujifunzayo yafikie moyo wetu, si masikio tu.

Soma kwa uangalifu sanduku lenye kichwa “Kuitambua Dini Yako Kuwa ya Kweli au ya Bandia.” Halafu jiulize hivi: ‘Je! sasa mimi naafiki kwamba kwa kadiri milki ya ulimwenguni pote ya dini bandia ihusikavyo, Voltaire alisema kweli alipoita dini “adui ya ainabinadamu”? Je! mtazamo huu mfupi katika historia ya kidini umenisaidia kuitambua dini ya kweli, na je! katika kipindi hiki cha wakati uliosonga sana katika mambo ya kibinadamu mimi najua mahali iwezapo kupatikana? Ikiwa ndivyo, je! nataka kuwa kama mtu yule aliyeelezwa na mwanainsha Mfaransa wa karne ya 18 Joseph Joubert, ambaye “ndani yayo yeye hupata shangwe yake na wajibu wake”?’

Wale wote wanaojibu ndiyo kwa maswali yaliyo juu na waendelee kunufaika kwa kusoma Amkeni! na vichapo viandamani vyalo. Sisi tungekualika ufuate ushauri wenye hekima utolewao na Zion’s Watch Tower lililotajwa juu: “Usiridhike na ua moja la ukweli. Kama moja lingalitosha kusingalikuwa na mengi zaidi. Yakusanye wakati wote, tafuta mengi zaidi.”

Ndiyo, endelea kukusanya, endelea kutafuta—tafuta mengi zaidi ya yale mazuri ya milele ya dini ya kweli!

[Sanduku katika ukurasa wa 18]

Kutambua Dini Yako Kuwa ya Kweli au ya Bandia

◼ Dini ya kweli huvuvia katika waabudu wayo kifungo kisichovunjika cha upendo na mwungamano kisichoathiriwa na mipaka ya kitaifa. (Yohana 13:35) Dini bandia haivuvii upendo wa jinsi hiyo. Bali, kwa kumwiga Kaini, washiriki wayo huenda na kuuana katika vita vya kimataifa.—1 Yohana 3:10-12.

◼ Dini ya kweli huendelea kuwa huru na siasa na humtegemea Muumba atatue matatizo ya ulimwengu kwa njia ya serikali yake ya Ufalme. Dini bandia hufuata kielelezo cha Nimrodi kwenye Mnara wa Babeli. Hujichanganya na siasa, hutumainia miungu ya kisiasa na kujiingiza-ingiza katika mambo yayo, na hivyo huweka msingi wa uharibifu wayo yenyewe.—Danieli 2:44; Yohana 18:36; Yakobo 1:27.

◼ Dini ya kweli humtambua Yehova kuwa Mungu wa kweli, yule wa pekee awezaye kukomboa kutoka kwenye uonevu. Dini bandia, kama ile iliyozoewa katika Misri na Ugiriki ya kale, ina umati wa miungu hoi ya kihadithi tu ambayo yote haina ustahili.—Isaya 42:5; 1 Wakorintho 8:5, 6.

◼ Dini ya kweli huahidi uhai wa milele duniani katika furaha. Dini bandia—kwa kielelezo, Ubuddha—huona maisha duniani kuwa yasiyotamanika na kuwa kitu cha kukombolewa nacho katika muda wa baadaye usio na uhakika.—Zaburi 37:29; Ufunuo 21:3, 4.

◼ Dini ya kweli, kwa njia ya kitabu chayo kitakatifu, Biblia, hujaza watu imani isiyotikisika; huwapa tumaini lililohakikishwa na kuwamotisha wawe na vitendo vya upendo halisi kuelekea Mungu na jirani. (2 Timotheo 3:16, 17) Dini bandia, ijapokuwa na vitabu vyayo vitakatifu, kwa sehemu kubwa haina matokeo katika kufanya mambo haya.—1 Yohana 5:3, 4.

◼ Dini ya kweli ina alama ya kuwa na waangalizi wanyenyekevu. Dini bandia yajulikana kwa kuwa na viongozi wenye kutaka makuu walio na akili za kujitegemea, walio na nia ya kupotosha ukweli na ambao hutafuta pato la kisiasa au la kilimwengu.—Matendo 20:28, 29; 1 Petro 5:2, 3.

◼ Dini ya kweli, ambayo ndiyo njia ya kunyenyekea Mungu ifaavyo, hutumia upanga wa kiroho, si halisi. Dini bandia, kwa upande mwingine, huridhiana mafundisho ya kweli, huvunja kutokuwamo kwa Kikristo, na hufuatia mahangaikio ya kibinadamu zaidi ya mapendezi ya kimungu.—2 Wakorintho 10:3-5.

◼ Dini ya kweli huvuta mioyo ya wasioamini kwenye ibada ya Mungu wa kweli. Dini bandia huchangia hali ya kutia shaka, fikira za kujitegemea binafsi, kufuata akili za binadamu tu, na kufuata mambo ya ulimwengu tu.—Luka 1:17; 1 Wakorintho 14:24, 25.

◼ Dini ya kweli, kama izoewavyo na Mashahidi wa Yehova, sasa inasitawi sana kiroho zaidi ya wakati wowote uliotangulia. Dini bandia, ikiwa na marinda yaliyopakwa-pakwa damu, inateseka kwa kukosa mlo wa kiroho na kupungukiwa na wenye kuiunga mkono.—Isaya 65:13, 14.

Ni nini wakati ujao wa dini kwa kutegemea wakati wayo uliopita? Dini bandia haina wakati ujao. Iache kabisa! (Ufunuo 18:4, 5) Geukia dini ya kweli. Hiyo itadumu milele.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki