Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g96 11/8 kur. 8-9
  • Dini Moja Itabaki

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Dini Moja Itabaki
  • Amkeni!—1996
  • Habari Zinazolingana
  • Chanzo cha Moyo Mkuu wa Daima
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Kuzoea Dini Safi Kwa Ajili Ya Kuokolewa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Je, Mungu Huzikubali Dini Zote?
    Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?
  • Kujiweka Huru Na Dini Bandia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1996
g96 11/8 kur. 8-9

Dini Moja Itabaki

EBU wazia jinsi hali ingekuwa ikiwa watu wote wa ulimwengu wangeungana katika dini moja, katika ibada moja safi ya Mungu wa pekee wa kweli. Hiyo ingekuwa chanzo cha muungano kama nini! Hakungekuwa tena ugomvi, zogo, au vita vya kidini. Je, hiyo ni ndoto tu? La. Ono la mtume Yohana la uharibifu wa yule kahaba, milki ya ulimwengu ya dini isiyo ya kweli, laonyesha kwamba aina moja ya ibada itabaki baada ya uharibifu wake. Ni gani hiyo?

Sauti aliyoisikia Yohana kutoka mbinguni yatoa dokezo: “Tokeni kwake, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake.” (Ufunuo 18:4) Ni wazi kwamba ni Mungu mwenyewe anayeongea hapa na watu wake. Ona kwamba haamuru watu wake wachangamane na yule kahaba katika jitihada ya pamoja ili kumwokoa kwa kumsaidia kujirekebisha kwa maisha bora. La, huyo kahaba hawezi kuponywa. Basi, Mungu awaamuru watoke kwake na kukaa mbali naye ili wasije wakachafuliwa na dhambi zake mbaya sana na kuepuka hatimaye kuhukumiwa na kuangamizwa pamoja naye.

Amri ya kimbingu ya ‘kutoka kwake’ pia husaidia watafutaji wa kweli wenye mioyo myeupe kutambulisha watu wa Mungu. Huenda wao wakajiuliza, ‘Ni watu gani leo duniani ambao wametii amri ya kutoka kwenye dini yoyote, shirika lolote, au kikundi chochote cha waabudu kinachohusika na “Babiloni Mkubwa”? (Ufunuo 18:2) Ni watu gani leo duniani ambao wameacha kabisa mafundisho, itikadi, mazoea, na mapokeo ya Kibabiloni?’ Wanaweza kuwa nani wengine ila Mashahidi wa Yehova? Miongoni mwa Mashahidi wanaozidi milioni 5.2 katika nchi zinazozidi 230, wale wote ambao walikuwa wameshirikishwa na dini fulani ya Kibabiloni, ama kwa uzaliwa ama kwa kugeuzwa imani, wamejiondoa kabisa huko—nyakati nyingine japo mateto na upinzani kutoka kwa watu wa ukoo, marafiki, na viongozi wa kidini.

Kielelezo kimoja ni Henry, mtu fulani wa Afrika Kusini, ambaye alikuwa mweka-hazina wa kanisa lake na ambaye alishikamana sana nalo. Lakini alikuwa akitafuta kweli, na siku moja alikubali funzo la Biblia la nyumbani bila malipo pamoja na Mashahidi wa Yehova. Baada ya muda, alipoamua kuwa Shahidi, alimwambia pasta, aliyekuwa pia jirani wake wa karibu, kwamba alitaka kujiuzulu kutoka kwenye kanisa.

Pasta huyo alishangaa na baadaye akachukua msimamizi wa kanisa na washiriki wengine wa kanisa kwenda kumzuru Henry. Waliuliza ni kwa nini alikuwa ameacha kanisa lao ili kuwa mshiriki wa dini ambayo, kulingana nao, haina roho takatifu ya Mungu. “Kwanza niliogopa kuwajibu,” akasema Henry, “kwa sababu sikuzote walikuwa na uvutano mkubwa juu yangu. Lakini nilisali kwa Yehova anipe msaada, naye aliniwezesha kujitetea hivi: ‘Kati ya dini zote za kimataifa, ni gani pekee ambayo hutumia kwa ukawaida jina la Mungu, Yehova? Je, si Mashahidi wa Yehova? Je, wafikiria Mungu atawaruhusu kutumia jina lake na asiwape roho yake takatifu?’” Wakuu wa kanisa hilo walishindwa kuthibitisha hoja hiyo kuwa uwongo, na Henry sasa ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova.

Hivyo, hiyo sauti kutoka mbinguni iamurupo: “Tokeni kwake,” kuna mahali pa kwenda. (Ufunuo 18:4) Kuna watu, waabudu wa Mungu wa kweli, Yehova, ambao unaweza kuwatorokea. Mamilioni yametoroka. Wakiitwa Mashahidi wa Yehova, wao hufanyiza udugu wa kimataifa wa Kikristo, wakiwa wamepangwa kitengenezo katika makutaniko zaidi ya 78,600, na ambao sasa wanapata ukuzi mkubwa zaidi katika historia. Wao wamebatiza zaidi ya watu 1,200,000 katika miaka minne iliyopita! Kabla ya ubatizo, wote hawa walikuwa wamemaliza mtaala wenye kuchochea kiroho wa funzo la Biblia, ukiwawezesha kufanya uamuzi mzuri wa binafsi wa kujiuzulu kutoka kwenye ushirika wowote ule wa zamani na dini nyingineyo yote.—Sefania 2:2, 3.

Ikiwa hujapata kuhudhuria mkutano wowote wa Mashahidi wa Yehova kwenye mojawapo Majumba ya Ufalme yao, mbona usihudhurie juma hili? Unaweza kuvutiwa na yale utakayoyaona na kusikia. Na ukitaka kuelewa Biblia, mbona usiombe mmoja wa Mashahidi wa Yehova ajifunze pamoja nawe, kama ambavyo mamilioni ya watu wengine wamefanya? Ikiwa sala yako ni kupata uelewevu wa kweli wa Neno la Mungu pamoja na njia ya maisha ambayo inapatana na Neno hilo, utapata majibu ya sala yako.

[Picha katika ukurasa wa 9]

Mamilioni yanageukia ibada ya Yehova Mungu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki