“Nahitaji Kitia-Moyo na Tumaini”
Je, wewe hujisikia hivyo wakati mwingine? Watu wengi leo hujisikia hivyo. Mwanamke mmoja kutoka Fort Smith, Arkansas, aliandikia makao makuu ya ulimwengu ya Mashahidi wa Yehova katika Brooklyn, New York, na alieleza:
“Kitabu chenu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele ni chenye kuelimisha sana na chenye kuchochea. Kwa siku chache, nilikisoma chote. Chanipa tumaini kwamba karibuni ulimwengu mpya ulioahidiwa chini ya utawala wa Yesu Kristo utakuja. Natamani siku hiyo.
“Mpaka wakati huo, ninakabiliwa na kusalimika katika ulimwengu huu, nikingojea huo uje. Mimi huvunjika moyo sana na maisha haya yasiyo na maana na yenye kuchosha ya kilimwengu. Nahitaji kitia-moyo na tumaini. Mlieleza kwamba ikiwa twapendezwa, kupitia tengenezo lenu twaweza kupata funzo la Biblia la nyumbani bila malipo. Tafadhali mwaweza kunieleza napaswa kufanya nini ili kulipata? Nafikiri funzo hili la Biblia litasaidia kunitia moyo.”
Ikiwa ungependa kupokea nakala ya kitabu Ujuzi Uongozao kwenye Uhai Udumuo Milele au ungependa mtu fulani aongoze funzo la Biblia la nyumbani pamoja nawe, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au anwani ya karibu zaidi nawe iliyoorodheshwa kwenye ukurasa 5.