“Gazeti la Hali ya Juu”
Je, umepata kusoma gazeti la Amkeni!? Ungeikadiria nakala uliyo nayo mikononi mwako kuwa yenye thamani gani? Je, unapata makala hizo kuwa zenye kuelimisha, zenye kufanyiwa utafiti vizuri, na zenye picha nzuri?
Mwandishi mmoja mwenye kujitegemea kutoka Nigeria, Afrika aandika hivi: “Ingawa mimi si mmoja wa Mashahidi wa Yehova, mimi husoma kwa ukawaida gazeti la Amkeni! Gazeti la Amkeni! ni la hali ya juu. Kwangu, hilo ni chanzo cha habari nyingi. Msomaji asiyekuwa na ubaguzi hupata hamu ya kufungua kurasa zake aonapo majalada yake yenye kuvutia. Kila toleo huonyesha uthibitisho wa ubunifu wenye kutokeza sana; kila ukurasa, uandishi bora. Kila toleo lina habari yenye thamani sana, likiwa na makala zilizochapishwa kwa wakati wake na zilizoandikwa vizuri sana.”
Twakutia moyo uchunguze makala zilizo katika nakala hii ya Amkeni! Ikiwa ungependa kupata nakala nyingine, tafadhali toa ombi lako kwa kuandikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya au tumia anwani ihusuyo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5. Tutafurahi kukupelekea nakala nyingine, au waweza kuomba mtu fulani akutembelee nyumbani mwako ili achunguze pamoja nawe umaana wa nyakati tunazoishi.