Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g98 10/22 uku. 32
  • ‘Nangojea kwa Hamu Paradiso Inayokuja’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Nangojea kwa Hamu Paradiso Inayokuja’
  • Amkeni!—1998
Amkeni!—1998
g98 10/22 uku. 32

‘Nangojea kwa Hamu Paradiso Inayokuja’

Ndivyo kijana mwenye umri wa miaka 14 anayeitwa Aleksandr alivyosema katika barua aliyoandikia ofisi ya tawi ya Watch Tower Society ya Urusi. Kijana huyu Mrusi alikuwa amepewa nakala za Mnara wa Mlinzi na fasihi nyingine zinazochapishwa na Mashahidi wa Yehova. Alieleza hivi katika barua yake:

“Niliposafiri na wazazi wangu hadi Khabarovsk kwa gari-moshi, tulifikiwa na Mashahidi wa Yehova. Walituambia mambo mengi kuhusu unabii wa Biblia, siku za mwisho, na uhai wa milele duniani.”

Kijana huyo alimalizia hivi: “Jinsi inavyopendeza kutambua kwamba karibuni uovu utakoma na kwamba watu wataishi milele duniani! Nangojea kwa hamu wakati dunia itakapogeuzwa iwe paradiso maridadi. Ningethamini sana ikiwa mngeniandikia kuhusu namna mafunzo ya Biblia yanavyoongozwa.”

Labda wewe pia unatamani ujuzi zaidi kuhusu makusudi ya Mungu. Ikiwa ndivyo, tafadhali jaza kuponi iliyo chini na kuipeleka kwa I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au kwa kutumia anwani ihusuyo katika ukurasa wa 5.

□ Nipelekeeni nakala ya broshua Mungu Anataka Tufanye Nini?

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki