“Ni Habari Bora Kama Nini!”
Vijana wanaweza kupataje kusudi maishani, kuelewa hali yao, au kujifunza kupatana na wazazi wao? Majuzi, ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova huko Hispania ilipokea barua, iliyosema hivi kwa sehemu:
“Kusudi langu la kuandika ni kuwapongeza sana kwa ajili ya kazi yenu inayostahili pongezi ya kuchapisha vitabu bora ajabu, kama kile kinachoitwa Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi. Ni habari bora kama nini! Nawapongeza waandishi na wachapishaji, ambao wametatua matatizo ya maelfu ya vijana.
“Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 21 ambaye amewahi kutafuta na kujifunza Biblia. . . . Bila kutarajia, nilipata kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi kupitia rafiki yangu.
“Mwanzoni nilifikiri kwamba hakingenisaidia, lakini hatua kwa hatua, nilipendezwa kukisoma. Kilinifanya nifikirie mambo mengi, kama vile ninachopaswa kufanya maishani, na hatua kwa hatua kilijibu maswali yangu. Nikiwa na hazina hiyo mikononi, nilijifunza jinsi niwezavyo kuwaelewa wazazi wangu, jinsi ya kusamehe, na jinsi ya kusitawisha sifa za kike na kutenda kama mwanamke.”
Ikiwa ungependa kunufaika na habari iliyomo katika kitabu Vijana Huuliza, unaweza kupokea nakala kwa kujaza na kupeleka kuponi iliyopo hapa kwa anwani iliyoonyeshwa kwenye kuponi au kwa anwani inayofaa iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.
□ Nipelekeeni kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi.
□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.