Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g03 9/8 uku. 19
  • Insha Yake Ilivutia Kwelikweli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Insha Yake Ilivutia Kwelikweli
  • Amkeni!—2003
  • Habari Zinazolingana
  • Alifanikiwa Kuliko Alivyotarajia
    Amkeni!—2003
  • “Waathiriwa Waliosahauliwa” Wakumbukwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Yehova Hatasahau Kazi Yenu Enyi Vijana!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Ninawezaje Kuwa na Uhusiano Mzuri na Mwalimu Wangu?
    Vijana Huuliza
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2003
g03 9/8 uku. 19

Insha Yake Ilivutia Kwelikweli

Alipokuwa katika mwaka wake wa mwisho, Ginny, mmoja wa Mashahidi wa Yehova huko Marekani, alipata fursa nzuri ya kuzungumza kuhusu dini yake. “Mwalimu alituambia kwamba tulihitaji kuandika insha ya mwisho ili tuhitimu,” akasema. “Nilimwambia kwamba ningependa kuandika kuhusu Mashahidi wa Yehova katika kambi za mateso za Nazi.”

Mwalimu alimpa Ginny ruhusa ya kuandika juu ya kichwa hicho. “Nilikuwa na wasiwasi wakati ulipofika wa kuwasilisha insha yangu na kuhutubia darasa,” akiri Ginny. “Sikujua kile ambacho wanafunzi wenzangu wangesema au kama wangenidhihaki.”

Ginny alianza hotuba yake kwa kuuliza hivi: “Je, kuna mtu yeyote anayejua ni nani waliovalia Nyota ya Daudi katika kambi za mateso za Nazi?” Kila mtu akajibu, “Ni Wayahudi.” Kisha akauliza kama kuna yeyote aliyejua ni nani waliovalia pembetatu ya zambarau. Hakuna aliyejibu. “Nikawaambia ni Mashahidi wa Yehova,” asema Ginny.

Mwalimu na wanafunzi walivutiwa sana na habari za Ginny. “Walistaajabu sana kujua kwamba Mashahidi wa Yehova wangeweza kuachiliwa kwa kutia tu sahihi kikaratasi fulani ili kukana imani yao,” asema Ginny. “Baadhi ya wanafunzi wenzangu waliniambia baadaye kwamba awali walikuwa wakiwadhihaki Mashahidi wa Yehova lakini wakati ujao watawasikiliza wakiwatembelea nyumbani kwao.”

Ginny alipata alama nne za A kwa ajili ya ripoti yake na hotuba yake. “Sikupata alama nzuri tu,” asema, “bali pia nilipata fursa nzuri ya kuongea kuhusu imani yangu!”

[Picha katika ukurasa wa 19]

Mashahidi wengi wa Yehova walipewa fursa ya kuachiliwa maadamu tu wangetia sahihi hati hii ya kukana imani yao

[Hisani]

Courtesy of United States Holocaust Memorial Museum

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki