Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g17 Na. 4 kur. 14-15
  • Kishawishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kishawishi
  • Amkeni!—2017
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kishawishi ni nini?
  • Kwa nini ni jambo la hekima kuepuka kishawishi haraka?
  • Unaweza kujiimarishaje ili ushinde vishawishi?
  • Jinsi ya Kupinga Vishawishi
    Amkeni!—2014
  • Kushinda Udhaifu wa Kibinadamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Ninaweza Kupinga Vishawishi Jinsi Gani?
    Vijana Huuliza
  • Unaweza Kupinga Kishawishi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2017
g17 Na. 4 kur. 14-15
Mwanamume akishawishiwa kwa gari maridadi, sigara, chakula, mwanamke, na pesa

MAONI YA BIBLIA

Kishawishi

Ndoa zilizovunjika, magonjwa, na dhamiri chafu ni mifano michache tu ya matokeo mabaya ya kushindwa na kishawishi. Tunaweza kuepukaje mtego huo?

Kishawishi ni nini?

Mtu hushawishiwa pale anapotamani kitu fulani, hasa kisichofaa. Fikiria mfano huu: Unaponunua vitu, unaona kitu chenye kuvutia. Unapata wazo la kwamba unaweza kuiba na usikamatwe. Hata hivyo, dhamiri yako inakukataza! Kwa hiyo, unapuuza wazo hilo na kusonga mbele. Kufikia hapo, unakuwa umefaulu kukishinda kishawishi.

BIBLIA INASEMA NINI?

Kushawishiwa hakumaanishi kwamba wewe ni mtu mbaya. Biblia inasema kwamba sisi sote hukabili vishawishi. (1 Wakorintho 10:13) Jambo muhimu ni jinsi tunavyotenda tunaposhawishiwa. Baadhi ya watu huiruhusu tamaa mbaya iwaathiri na hatimaye kutumbukia kwenye dhambi. Wengine hutambua kishawishi mapema na kukiepuka mara moja.

“Kila mtu hujaribiwa kwa kuvutwa na kushawishiwa na tamaa yake mwenyewe.”—Yakobo 1:14.

Kwa nini ni jambo la hekima kuepuka kishawishi haraka?

Biblia inafunua hatua ambazo huongoza kwenye dhambi. Yakobo 1:15 inasema: “Kisha tamaa [mbaya], wakati imetunga mimba, huzaa dhambi.” Kwa ufupi, kuendelea kufikiria mambo mabaya hufanya mtu afikie hatua ambayo hawezi kabisa kujizuia, kama vile mama mjamzito aliyefikia hatua ya kujifungua. Hata hivyo, tunaweza kuepuka kuwa watumwa wa tamaa mbaya. Tunaweza kushinda.

JINSI BIBLIA INAVYOWEZA KUKUSAIDIA

Kama tu akili yetu inavyoweza kuruhusu mawazo mabaya yaingie, ndivyo pia inavyoweza kuyaondoa. Jinsi gani? Kwa kukazia fikira jambo lingine, kama vile utendaji fulani, mazungumzo na rafiki, au wazo lenye kujenga. (Wafilipi 4:8) Ni muhimu pia kufikiria matokeo ya kushindwa na jaribu, ambayo yanaweza kutia ndani madhara ya kimwili, kihisia, au ya kiroho. (Kumbukumbu la Torati 32:29) Sala pia inaweza kukusaidia sana. Yesu Kristo alisema hivi: “Endeleeni . . . kusali sikuzote, ili msiingie katika jaribu.”—Mathayo 26:41.

“Msipotoshwe: Mungu si wa kudhihakiwa. Kwa maana lolote lile analopanda mtu, atavuna hilo pia.”—Wagalatia 6:7.

Unaweza kujiimarishaje ili ushinde vishawishi?

UKWELI WA MAMBO

Kumbuka kwamba kishawishi ni mtego ambao unaweza kusababisha madhara kwa mtu asiye na busara au asiye makini. (Yakobo 1:14) Ukweli huo ni wazi zaidi hasa kwa vishawishi vinavyohusisha uasherati, ambavyo hutokeza madhara makubwa sana.—Methali 7:22, 23.

JINSI BIBLIA INAVYOWEZA KUKUSAIDIA

Yesu Kristo alisema hivi: “Ikiwa, sasa, hilo jicho lako la kuume linakufanya ukwazike, ling’oe ulitupilie mbali nawe.” (Mathayo 5:29) Ni wazi kwamba Yesu hakumaanisha tung’oe jicho kihalisi! Badala yake, alimaanisha kwamba ni lazima tuue viungo vya mwili wetu kuhusiana na kufanya dhambi ikiwa tunataka kumpendeza Mungu na kupata uzima wa milele. (Wakolosai 3:5) Hilo linamaanisha kuchukua hatua madhubuti ili kupinga jaribu. Mwanamume fulani mwaminifu alisali hivi kwa Mungu: “Uyafanye macho yangu yapite ili yasione jambo lisilofaa.”—Zaburi 119:37.

Ni kweli kwamba huenda isiwe rahisi kujizuia. Biblia inasema “mwili ni dhaifu.” (Mathayo 26:41) Hivyo, huenda tukafanya makosa. Hata hivyo, tunapotubu kikweli na kujitahidi kuepuka zoea la kufanya dhambi, Muumba wetu, Yehova Mungu, atakuwa “mwenye rehema na mwenye neema” kutuelekea. (Zaburi 103:8) Jambo hilo linatia moyo kwelikweli!

“Kama ungekuwa unaangalia makosa, Ee Yah, Ee Yehova, ni nani angesimama?” —Zaburi 130:3.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki