Yehova Anatupatia Mwokozi
29 Mtu wa kwanza wa kiroho kuumbwa na Mungu alikuwa kwake kama mwana mzaliwa wa kwanza.
Mungu anampenda huyo sana na atamtunia kuharibu wabaya na kuokoa wanaotii.—Yohana 3:16, 36
30 Yehova alituma Mwana wake azaliwe duniani. Aliitwa Yesu. Jina la mama yake lilikuwa Mariamu.—Luka 1:30-35
31 Wakati Yesu alipokuwa mkubwa alifundisha watu mambo mengi mazuri. Aliwafundisha kwamba Yehova peke yake ndiye Mungu wa kweli.—Marko 12:29, 30, tafsiri ya Biblia ya New World
Yesu alisema inatupasa kuabudu Yehova peke yake.—Mathayo 4:10; Yohana 4:23, 24
Vilevile alifundisha watu habari za ufalme wa Yehova.—Luka 17:20, 21, tafsiri ya Biblia ya New World
32 Yesu aliponesha wagonjwa na kufanya mambo mengi mema. Yeye hakufanya mabaya.—Matendo 10:38; 1 Petro 2:21, 22
Lakini yeye angetuokoa namna gani katika dhambi na kifo?
33 Ilikuwa lazima atolee Mungu dhabihu (sadaka) ili aokoe watu wema. Zamani za kale, Mungu aliambia watu wachinje wanyama wawe dhabihu (sadaka) kwa ajili ya dhambi zao.—Waebrania 7:25, 27
34 Yesu hakuchinja wanyama wawe dhabihu. Yeye alijitoa mwenyewe awe dhabihu kwa ajili yetu.—Mathayo 20:28; Waebrania 10:12
Wewe unajua sababu?