Namna Sisi Tunaokolewa Katika Dhambi na Kifo
35 Wewe unakumbuka kwamba Adamu, yule mtu wa kwanza, alifanya dhambi? Alipoteza uzima na paradiso, na sisi sote tunakufa pia, kwa sababu sisi ni watoto wake.—Warumi 5:12; 3:23
36 Tungeweza kupata tena uzima huo mkamilifu, kama mwanadamu mwingine mkamilifu angetoa uhai wake kwa ajili yetu, au atukomboe katika kifo.—1 Wakorintho 15:45; Warumi 5:19, 21
37 Yesu alikuwa Mwana wa Mungu. Alikuwa mwanadamu mkamilifu. Yeye hakufanya dhambi.—Waebrania 5:9; 7:26
38 Alikubali kuuawa na watu ambao hawakupenda Mungu.—Matendo 2:23
Kwa kufanya hivyo yeye alijitoa mwenyewe awe dhabihu kwa ajili yetu.—1 Timotheo 2:6
39 Yesu alizikwa katika pango au kaburi ambalo lilichongwa katika mwamba (jiwe kubwa). Aliendelea kuwa mfu kwa siku tatu. Halafu Mungu akamfufua.—Matendo 2:24
40 Alirudi mbinguni. Sasa yeye anaweza kuomba Mungu asaidie wale wanaotii Mungu.—Waebrania 9:24; 1 Yohana 2:1, 2