Tunakualika
Tumefurahia kusema nawe kupitia broshua hii. Twatumaini umefurahia kujifunza mengi zaidi juu ya Mashahidi wa Yehova. Tafadhali kubali mwaliko wetu wa kututembelea kwenye Jumba letu la Ufalme. Ujionee jinsi mikutano yetu inavyofanywa. Ujionee jinsi tunavyojitahidi kuwajulisha wengine habari njema za dunia paradiso chini ya Ufalme wa Kristo.
Mungu ameiahidi. “Ziko mbingu mpya na dunia mpya ambazo tunangojea kulingana na ahadi yake, na katika hizo uadilifu utakaa.” (2 Petro 3:13) Karne nyingi zimepita. Muda wa kusubiri wakaribia kwisha. Hali za ulimwengu zaonyesha hivyo.
“Kadiri mwonavyo siku ikikaribia,” akasema mtume Paulo, “tufikiriane ili kuchocheana kwenye upendo na kazi zilizo bora, si kuachilia mbali kukusanyika pamoja sisi wenyewe.” (Waebrania 10:24, 25) Sisi twakualika ufuate ushauri wa Paulo ukutanike pamoja nasi.