Mwaliko Wetu Kwako
Tumefurahia kusema nawe kupitia kurasa za broshua hii. Twatumaini umefurahia kujifunza mengi zaidi juu ya Mashahidi wa Yehova. Tafadhali kubali mwaliko wetu wa kututembelea kwenye Jumba la Ufalme letu. Ona jinsi mikutano yetu inavyoongozwa. Ona jinsi tunavyojitahidi kushiriki pamoja na wengine habari njema za dunia-paradiso chini ya Ufalme wa Kristo.
Mungu ameiahidi. “Ziko mbingu mpya na dunia mpya ambazo sisi tunangojea kulingana na ahadi yake, na katika hizo uadilifu utakaa.” (2 Petro 3:13, New World Translation) Karne kumi na tisa zimepita. Muda wa kusubiri wakaribia mwisho. Hali za ulimwengu zaonyesha hivyo. Utimizo wa ahadi hii ya Yesu wakaribia: “Mambo hayo yaanzapo kutokea, changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia.”—Luka 21:28.
“Kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia,” akasema mtume Paulo, “tukaangaliane sisi kwa sisi na kuhimizana katika upendo na kazi nzuri; wala tusiache kukusanyika pamoja.” (Waebrania 10:24, 25) Sisi twakutolea mwaliko wa kwamba, Fuata ushauri wa Paulo kwa kukusanyika pamoja nasi.