Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g95 6/22 uku. 13
  • Fulizeni Kuwa Tayari kwa Wakati Ujao Mwangavu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Fulizeni Kuwa Tayari kwa Wakati Ujao Mwangavu
  • Amkeni!—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Mwaliko Wetu Kwako
    Mashahidi wa Yehova Katika Karne ya 20
  • Tayarisha kwa Ajili ya Kukombolewa Kuingia Ndani ya Ulimwengu Mpya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Jipeni Moyo Kadiri Ukombozi Ukaribiavyo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Je, Uko Tayari kwa Siku ya Yehova?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1995
g95 6/22 uku. 13

Fulizeni Kuwa Tayari kwa Wakati Ujao Mwangavu

“FULIZENI kuwa tayari,” Yesu alisihi. (Luka 12:40, NW) Ikiwa tutafanya hivyo, Kristo ajapo “pamoja na nguvu na utukufu mwingi,” tutaweza kuitikia kwa shangwe amri yake: “Changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia.”—Luka 21:27, 28.

Ukombozi wa aina gani? Ah, aina ya ukombozi aliyofurahia Noa na familia yake—ndiyo, kupitia mwisho wa ulimwengu huu! “Ulimwengu unapitilia mbali,” aliandika mtume Yohana, “lakini yeye afanyaye mapenzi ya Mungu hudumu milele.”—1 Yohana 2:17, NW.

Katika ulimwengu mpya wa Yehova, raia wa kidunia wa Mfalme, Yesu Kristo, watafurahia uhai udumuo milele. “Wenye haki watairithi nchi,” Biblia yasema, “nao watakaa humo milele.” (Zaburi 37:29) Ni wakati ujao wenye kupendeza kama nini ambao Mungu aahidi watu wake! “Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao,” lasema Neno lake. “Atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena.” Huu ni unabii wa kweli!—Ufunuo 21:3, 4.

Lakini, ili kufurahia wakati ujao huu, lazima utende. Kupata ujuzi ni jambo la kwanza la lazima. Biblia huelezea hivi: “Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.”—Yohana 17:3.

Unahitaji pia kukutana kwa ukawaida pamoja na wengine ambao wanatafuta ujuzi huu, kama alivyosihi mtume: “Tukaangaliane sisi kwa sisi na kuhimizana katika upendo na kazi nzuri; wala tusiache kukusanyika pamoja . . . kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.” (Waebrania 10:24, 25) Kwa hakika, watu wa Yehova wanaona ile siku ya kukombolewa kuingia katika ulimwengu mpya wa Mungu ikiwa karibu zaidi kuliko wakati mwingineo wote, na ndivyo wamejulikana kwa kukutana kwao pamoja.

Likitoa maelezo juu ya kusanyiko moja kwenye stediamu moja kubwa, Sunday Telegraph la London liliripoti hivi: “Hakuna lolote baya na kile kinachohusianishwa kidesturi na wale wanaotangaza kwamba ‘Mwisho Uko Karibu.’ Huenda Mashahidi wakaamini kwamba mwisho uko karibu. Hata hivyo, kwa wakati uliopo kila mtu aonekana akijifurahisha katika njia ya kiasi, iliyo adilifu, na ya Kimungu lakini yenye uchangamfu.” Halafu gazeti hilo likaongeza hivi: “Ikiwa mfumo wa sasa wa ulimwengu kwa kweli uko karibu kuangamia, Mashahidi katika Twickenham waonekana wakiwa tayari kabisa kupanga mwingine mpya.”

Kufuliza kuwa tayari humaanisha kufuliza kuwa wenye shughuli, katika kufanya kazi kama ile iliyofanywa na Noa, ambaye alitumikia katika zile siku za kabla ya Furiko akiwa “mhubiri wa uadilifu.” (2 Petro 2:5, NW) Kufuliza kuwa tayari humaanisha pia kujihusisha “katika matendo matakatifu ya mwenendo na vitendo vya ujitoaji kimungu.” Unakaribishwa, ndiyo, unasihiwa, ujiunge na watu wa Yehova katika ‘kungojea na kuweka karibu akilini kuwapo kwa siku ya Yehova.’—2 Petro 3:11, 12, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki