Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 4/15 kur. 16-21
  • Tayarisha kwa Ajili ya Kukombolewa Kuingia Ndani ya Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tayarisha kwa Ajili ya Kukombolewa Kuingia Ndani ya Ulimwengu Mpya
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi Tunavyotenda kwa Kuitikia Njia ya Ulimwengu ya Maisha
  • Ni Nani au Ni Nini Huwa cha Kwanza Maishani?
  • Matayarisho Yenye Upendo kwa Ajili ya Ukombozi Mkubwa Zaidi
  • Sababu Kwa Nini Tendo la Kukata Maneno ni Muhimu Sasa
  • Msaada wa Kimungu kwa Kutazamia Ukombozi
  • Mkumbuke Mke wa Loti
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Mke wa Lutu Alitazama Nyuma
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Jipeni Moyo Kadiri Ukombozi Ukaribiavyo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Unapaswa Kuwa Wapi Mwisho Unapokuja?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 4/15 kur. 16-21

Tayarisha kwa Ajili ya Kukombolewa Kuingia Ndani ya Ulimwengu Mpya

“Kumbukeni mke wa Loti.”—LUKA 17:32, NW.

1. Somo letu leo linakazia kielelezo kipi cha kihistoria cha ukombozi wa kimungu, na kinaweza kutunufaishaje sisi?

BAADA ya kusimulia ule ukombozi mzuri ajabu ambao Yehova alifanya kwa ajili ya Noa na jamaa yake, mtume Petro alitaja kielelezo kingine cha kihistoria. Yeye alivuta uangalifu kwenye kuhifadhiwa kwa Loti mwadilifu wakati Sodoma na Gomora yalipofanywa kuwa majivu, kama tusomavyo kwenye 2 Petro 2:6-8. Mambo hayo mengimengi yalihifadhiwa kwa manufaa yetu. (Warumi 15:4) Kuzingatia yale yaliyotukia kuhusiana na ukombozi huo kunaweza kusaidia kutuweka katika mstari wa kuhifadhiwa na kuingia ndani ya ulimwengu mpya wa Mungu.

Jinsi Tunavyotenda kwa Kuitikia Njia ya Ulimwengu ya Maisha

2. Ni mwenendo gani katika Sodoma na Gomora uliongoza katika kuharibiwa kwao na Mungu?

2 Kwa nini majiji haya yaliharibiwa pamoja na wakaaji wayo? Mtume Petro anataja kujitia sana katika “mwenendo mlegevu.” (2 Petro 2:7, NW) Kama inavyoonyeshwa na utumizi wa neno la Kigiriki ambalo kutokana nalo usemi huo umetafsiriwa, watu wa Sodoma na Gomora walijitia sana katika kutenda makosa kwa njia iliyoonyesha ukosefu wa staha kwa kupindukia, hata dharau, kwa sheria na mamlaka. Yuda 7, NW husema kwamba “walifanya uasherati kupita kiasi” na ‘wakafuata mwili kwa matumizi yasiyo ya asili.’ Ubaya mwingi wa mwenendo wao ulidhihirika wakati “watu wa Sodoma, . . . vijana kwa wazee, watu wote waliotoka pande zote,” walipoizunguka nyumba ya Loti na kumwamuru awatoe wageni wake kwa watu wa Sodoma ili watosheleze tamaa zao zilizopotoka. Nao walimlaani Loti kwa sababu alikinza madai yao mapotovu.—Mwanzo 13:13; 19:4, 5, 9.

3. (a) Loti na jamaa yake walikujaje kuwa wanaishi katika mazingira yenye ufisadi kama Sodoma? (b) Itikio la Loti kwa mwenendo mlegevu wa watu wa Sodoma lilikuwaje?

3 Mwanzoni Loti alikuwa amehamia eneo lililoko karibu na Sodoma kwa sababu ya uwezekano walo wa ufanisi wa vitu vya kimwili. Baadaye, akaanza kukaa ndani ya jiji lenyewe. (Mwanzo 13:8-12; 14:12; 19:1) Lakini yeye hakukubaliana na mazoea machafu ya watu wa jiji hilo, na watu hao hawakumwona kuwa mmoja wao, kwa wazi ni kwa sababu Loti na jamaa yake hawakushiriki maisha yao ya kijamii. Kama vile 2 Petro 2:7, 8, NW husema: “Loti [alisumbuliwa] sana na anasa ya mwenendo mlegevu wa watu wakaidi-sheria—maana mtu huyo mwadilifu kwa yale aliyoona na kusikia alipokuwa akikaa miongoni mwao siku kwa siku, alikuwa akitesa nafsi yake yenye uadilifu kwa sababu ya matendo yao yasiyo ya kisheria.” Hali hizo zilileta jaribu kali kwa Loti kwa sababu, akiwa mtu mwadilifu, alikirihi mwenendo kama huo.

4. (a) Ni katika njia zipi hali leo ni kama zile zilizokuwa katika Sodoma la kale? (b) Ikiwa sisi tuko kama Loti mwadilifu, tunaitikiaje hali zenye ufisadi zilizopo?

4 Katika siku yetu pia, hali ya kiadili ya jamii ya kibinadamu imeshushwa sana. Katika mabara mengi, watu wengi zaidi na zaidi wanajitia katika ngono kabla ya ndoa au nje ya ndoa. Hata vijana wengi shuleni mara nyingi wanajihusisha sana katika njia hii ya maisha, nao wanadhihaki wale wasiojiunga nao. Wagoni-jinsia-moja wanajitambulisha waziwazi na wanafanya gwaride kupitia barabara za majiji makubwa wakidai watambuliwe. Makasisi wamejiunga katika kujifurahisha anasa hii. Kirasmi, si makanisa mengi huwafanya wagoni-jinsia-moja na waasherati kuwa makasisi. Hata hivyo, kihalisi, kama vile ripoti za magazetini zimeonyesha kwa kurudia-rudia, si vigumu sana kupata wagoni-jinsia-moja, waasherati, na wazinzi wakiwa miongoni mwa makasisi. Kwa hakika, viongozi fulani wa kidini wamehamishwa kupelekwa majiji mengine au hata wakalazimika kujiuzulu kwa sababu ya kashifa zinazohusu ngono. Wapenda uadilifu hawakubaliani na uovu huo; ‘wanakirihi lililo ovu.’ (Warumi 12:9, NW) Hasa wanahuzunika wakati mwenendo wa watu wanaodai kumtumikia Mungu unapoleta suto juu ya jina lake na kusababisha watu wasiojua kitu waachane na dini yote kwa kuchukizwa.—Warumi 2:24.

5. Ni swali gani linalojibiwa na kuharibiwa kwa Sodoma na Gomora na Yehova?

5 Mwaka baada ya mwaka hali huzidi kuwa mbaya. Je! utakuwako mwisho? Ndiyo, utakuwako! Alilofanya Yehova kwa Sodoma na Gomora ya kale huonyesha waziwazi kwamba, katika wakati wake uliowekwa, yeye atatekeleza hukumu. Ataharibu kabisa waovu, lakini atakomboa watumishi wake washikamanifu.

Ni Nani au Ni Nini Huwa cha Kwanza Maishani?

6. (a) Ni somo gani la wakati wake lililo katika habari juu ya vijana waliokuwa karibu kuoa binti za Loti? (b) Mtazamo wa hao waliotarajiwa kuwaoa ulitahinije binti za Loti?

6 Ni wale tu wanaodhihirisha ujitoaji kimungu wa kweli wataachiliwa. Kwa habari hii, fikiria yale ambayo malaika za Yehova walimwambia Loti kabla ya Sodoma na Gomora kuharibiwa. “Je! unaye mtu hapa zaidi, mkwe, wanao, na binti zako, na wo wote ulio nao katika mji, uwatoe katika mahali hapa; maana tutapaharibu sisi mahali hapa.” Kwa hiyo Loti akaondoka akaseme na wale vijana waliokuwa karibu kuoa binti zake. Alirudia-rudia kuwahimiza: “Ondokeni mtoke katika mahali hapa kwa sababu BWANA [Yehova, NW] atauharibu mji huu”! Uhusiano wao kwa jamaa ya Loti uliwatolea fursa ya pekee wakombolewe, lakini ilikuwa lazima wao binafsi wachukue hatua. Ilikuwa lazima waonyeshe ushuhuda wenye kuonekana wa utii kwa Yehova. Badala ya hivyo, machoni pao Loti “akawa kama achezaye.” (Mwanzo 19:12-14) Unaweza kuwazia walivyohisi binti za Loti walipojua jambo lililokuwa limetukia. Lilitahini ushikamanifu wao kwa Mungu.

7, 8. (a) Wakati malaika walipohimiza Loti achukue jamaa yake na kukimbia, aliitikiaje, na ni kwa nini hilo lilikuwa si jambo la hekima? (b) Ili wakombolewe, ni jambo gani lililokuwa muhimu kwa Loti na jamaa yake?

7 Kwenye mapambazuko ya kesho yake, wale malaika wakamhimiza Loti. Wakasema: “Ondoka, mtwae mkeo na binti zako wawili waliopo hapa, usipotee katika maovu ya mji huu”! Lakini ‘akakawia-kawia.’ (Mwanzo 19:15, 16) Kwa nini? Ni kitu gani kilichomkawiza? Je! ni vitu vya kimwili alivyokuwa navyo huko Sodoma—vile vitu hasa vilivyokuwa vimemvutia aje katika eneo hilo pale mwanzoni? Ikiwa angeshikamana navyo, angeharibiwa pamoja na Sodoma.

8 Kwa huruma, malaika wakawashika kwa mikono wale wa jamaa yake wakawaharakisha watoke ndani ya jiji. Walipokuwa viungani, malaika wa Yehova akaamuru: “Jiponye nafsi yako; usitazame nyuma, wala usisimame katika hilo bonde po pote; ujiponye mlimani, usije ukapotea”! Bado Loti alisita-sita. Mwishowe, baada ya kuafikiana kwamba angeweza kwenda mahali ambapo si mbali sana, yeye na jamaa yake wakakimbia. (Mwanzo 19:17-22) Hakungekuwa na kukawia zaidi; utii ulikuwa wa lazima kabisa.

9, 10. (a) Kwa nini kuwa na mume wake hakukutosha ili kuhifadhi mke wa Loti? (b) Wakati mke wa Loti alipouawa, ni mtihani gani zaidi ulioletwa juu ya Loti na binti zake?

9 Hata hivyo, ukombozi ulikuwa haujakamilika walipotoka Sodoma. Mwanzo 19:23-25 hutuambia hivi: “Jua lilikuwa limechomoza juu ya nchi Lutu [Loti, NW] alipoingia Zoari. Ndipo BWANA [Yehova, NW] akanyesha juu ya Sodoma na juu ya Gomora kiberiti na moto toka mbinguni kwa BWANA [Yehova, NW]. Akaangusha miji hiyo na Bonde lote, na wote waliokaa katika jiji hilo na yote yaliyomea katika nchi ile.” Lakini mke wa Loti alikuwa wapi?

10 Alikuwa amekimbia pamoja na mume wake. Hata hivyo, je! alikubaliana kabisa na aliyokuwa akifanya? Hakuna jambo lolote la kuonyesha kwamba alikubaliana na ukosefu wa adili wa Sodoma katika njia yoyote. Lakini je! upendo wake kwa Mungu ulikuwa imara zaidi ya ushikamano wake na kao lake na vitu vya kimwili alivyokuwa navyo humo? (Linganisha Luka 17:31, 32.) Akiwa chini ya mkazo, lililokuwa moyoni mwake likadhihirika. Kwa wazi tayari walikuwa karibu na Zoari, pengine katika hatua ya kuingia jijini, alipogeuka kwa kutokutii akatazama nyuma. Na kama vile maandishi ya Biblia husema, “akawa nguzo ya chumvi.” (Mwanzo 19:26) Sasa mtihani zaidi wa ushikamanifu ukakabili Loti na binti zake. Je! ushikamano wa Loti kwa mke wake mfu au ushikamano wa wale wasichana kwa mama yao aliyekufa ulikuwa imara zaidi ya upendo wao kwa Yehova, aliyeleta afa hili? Je! wangeendelea kutii Mungu hata ingawa mtu fulani aliye karibu sana nao alithibitika kuwa si mwenye ushikamanifu kwake? Wakiwa na tumaini kamili katika Yehova, wao hawakutazama nyuma.

11. Tumejifunza nini hapa juu ya ukombozi anaoandaa Yehova?

11 Ndiyo, Yehova ajua jinsi ya kukomboa watu wa ujitoaji kimungu katika jaribu. Ajua jinsi ya kukomboa jamaa nzima-nzima ambazo zimeungana katika ibada safi; ajua pia kukomboa watu mmoja mmoja. Wanapompenda kikweli, anaonyesha ufikirio mkubwa katika kushughulika nao. “Yeye anatujua umbo letu, na kukumbuka ya kuwa sisi tu mavumbi.” (Zaburi 103:13, 14) Lakini ukombozi wake ni wa wale tu walio watu wa ujitoaji kimungu, wale ambao ujitoaji wao ni wa kweli, wale ambo utii wao ni wonyesho wa ushikamanifu.

Matayarisho Yenye Upendo kwa Ajili ya Ukombozi Mkubwa Zaidi

12. Ni matayarisho gani yenye upendo ambayo Yehova angefanya kabla ya kuleta ukombozi ambao sisi tunatazamia kwa hamu?

12 Kwa yale aliyosababisha katika siku za Noa na Loti, Yehova hakuondoa waovu wote milele. Kama vile andiko lisemavyo, yaliweka kiolezo tu cha mambo yatakayokuja. Kabla ya mambo hayo kuwasili, Yehova alikuwa na mengi zaidi akilini mwake ambayo angefanya kunufaisha watu wanaompenda. Angetuma duniani Yesu Kristo, Mwana wake mzaliwa pekee. Hapa, Yesu angeondolea jina la Mungu malawama kwa kuonyesha aina ya ujitoaji ambao Adamu akiwa binadamu mkamilifu angalimtolea Mungu; lakini Yesu angefanya hivyo chini ya hali ngumu zaidi sana. Yesu angetoa uhai wake mkamilifu wa kibinadamu ukiwa dhabihu ili wazao wa Adamu ambao wangejizoeza imani waweze kuwa na kile Adamu alipoteza. Kisha, “kundi dogo” la binadamu washikamanifu wangechaguliwa na Mungu wakashiriki pamoja na Kristo katika Ufalme wake wa kimbingu, na umati mkubwa ungekusanywa kutoka katika mataifa yote wakawe msingi wa jamii mpya ya kibinadamu. (Luka 12:32; Ufunuo 7:9) Hayo yakiisha timizwa, Mungu angefanya ukombozi mkuu ambao matukio yaliyoshirikishwa na Gharika na uharibifu wa Sodoma na Gomora yalikuwa violezo.

Sababu Kwa Nini Tendo la Kukata Maneno ni Muhimu Sasa

13, 14. Tunaweza kujifunza nini kutokana na uhakika wa kwamba Petro alitumia uharibifu wa watu wasiohofu Mungu katika siku za Loti na za Noa kuwa vielelezo?

13 Wanafunzi wa Neno la Mungu wanajua kwamba katika pindi nyingi Yehova amefanya matendo ya ukombozi kwa ajili ya watumishi wake. Hata hivyo, katika visa vingi Biblia haisemi, ‘Kama ilivyokuwa wakati huo, ndivyo kuwapo kwa Mwana wa mtu kutakavyokuwa.’ Ni kwa nini mtume Petro, akivuviwa na roho takatifu, alitenga vielelezo viwili tu? Ni nini kilichokuwa tofauti juu ya yale yaliyotukia katika siku za Loti na za Noa?

14 Kionyeshi dhahiri kinapatikana kwenye Yuda 7, NW, tusomapo kwamba “Sodoma na Gomora na majiji yaliyokuwa karibu karibu nayo . . . yamewekwa mbele yetu sisi kama kielelezo cha kuonya kwa kupata adhabu ya kihukumu ya moto wa milele.” Ndiyo, uharibifu wa watenda dhambi hao wabaya sana katika majiji hayo ulikuwa wa milele, kama utakavyokuwa uharibifu wa waovu mwishoni mwa mfumo mwovu wa mambo uliopo. (Mathayo 25:46) Furiko la siku ya Noa vivyo hivyo linatajwa katika habari zinazozungumza hukumu za milele. (2 Petro 2:4, 5, 9-12; 3:5-7) Hivyo kwa uharibifu wa watu wasiohofu Mungu katika siku za Loti na za Noa, Yehova alionyesha kwamba yeye atakomboa watumishi wake kwa kuharibu milele watu ambao ni wazoevu wa ukosefu wa uadilifu.—2 Wathesalonike 1:6-10.

15. (a) Ni onyo gani muhimu linalotolewa kwa wale wanaojitia katika mazoea maovu? (b) Kwa nini haki itatekelezwa juu ya wote wanaodumu katika ukosefu wa uadilifu?

15 Uharibifu wa waovu haumfurahishi Yehova, wala haufurahishi watumishi wake. Kwa njia ya Mashahidi wake, Yehova huhimiza watu hivi: “Ghairini, ghairini, mkaache njia zenu mbaya; mbona mnataka kufa?” (Ezekieli 33:11) Ijapokuwa hivyo, wakati watu wanapoonyesha kwamba hawana tamaa ya kutii sihi hii yenye upendo bali wanadumu katika njia yao wenyewe ya maisha ya ubinafsi, staha ya Yehova kwa jina lake mwenyewe na upendo wake kwa watumishi wake wenye ushikamanifu wanaotendwa vibaya na watu wasiohofu Mungu hutaka kwamba atekeleze haki.

16. (a) Kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba ukombozi uliotabiriwa u karibu sana? (b) Ukombozi utakuwa kutoka nini na kuingia katika nini?

16 Wakati wa Mungu wa kuleta ukombozi u karibu sana! Mitazamo ya watu na matukio ambayo Yesu alitabiri kuwa ishara ya kuwapo kwake na ya umalizio wa mfumo wa mambo inaonekana waziwazi. Mambo mbalimbali ya ishara hiyo yalianza kuonekana kwanza karibu miaka 75 iliyopita, na Yesu alisema kwamba “kizazi hiki” hakingepita kamwe kabla ya Mungu kutekeleza hukumu juu ya ulimwengu huu usiohofu Mungu. Yehova aamuapo kwamba ujumbe wa Ufalme umepigiwa mbiu kwa kadiri ya kutosha katika dunia yote inayokaliwa kwa ajili ya ushahidi kwa mataifa yote, ndipo mwisho wa huu ulimwengu mwovu utakuja, na pamoja na huo utakuja ukombozi kwa ajili ya watu wa ujitoaji kimungu. (Mathayo 24:3-34; Luka 21:28-33) Kukombolewa na nini? Kukombolewa na majaribu ambayo wamelazimika kupatwa nayo mikononi mwa waovu, kukombolewa na hali ambazo zimekuwa kila siku chanzo cha dhiki kwao wakiwa wapenda uadilifu. Pia kutakuwa kukombolewa kuingizwa ndani ya ulimwengu mpya ambamo magonjwa na kifo vitakuwa vitu vya wakati uliopita.

Msaada wa Kimungu kwa Kutazamia Ukombozi

17. (a) Ni swali gani la makini tunalopaswa kujiuliza? (b) Sisi tunaweza kutoaje uthibitisho kwamba, kama Noa, tunasukumwa na “hofu ya kimungu”?

17 Swali ambalo sisi watu mmoja mmoja tunahitaji kufikiria ni, ‘Je! mimi niko tayari kwa tendo hilo la Mungu?’ Ikiwa sisi twajitegemea wenyewe au wazo letu wenyewe la uadilifu, basi hatuko tayari. Lakini, ikiwa kama Noa, tunasukumwa na “hofu ya kimungu,” basi tunaitikia kwa imani mwelekezo tunaopewa na Yehova, na hiyo itaongoza kwenye ukombozi wetu.—Waebrania 11:7, NW.

18. Kwa nini kujifunza staha inayofaa kwa mamlaka ya kitheokrasi ni sehemu yenye umaana ya utayarishaji wetu kwa ukombozi kuingia ndani ya ulimwengu mpya?

18 Ikiwaeleza vizuri wale ambao hushangilia ulinzi ambao Yehova hutoa hata sasa, Zaburi 91:1, 2, NW husema hivi: “Yeyote anayekaa katika mahali pa siri pa Aliye Juu Zaidi atajipatia mwenyewe makao chini ya uvuli wenyewe wa Mmoja Mweza Yote. Nitasema kwa Yehova: ‘Wewe ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, nitakayetegemea.’” Hapa pana kikundi cha watu wanaolindwa na Mungu kama vifaranga chini ya mabawa yenye nguvu ya ndege mzazi. Tumaini lao kamili limo katika Yehova. Wanakiri kwamba ndiye Aliye Juu Zaidi, Mmoja Mweza Yote. Kama tokeo, wanastahi mamlaka ya kitheokrasi na kujitiisha chini yayo wao wenyewe, iwe inatumiwa na wazazi au na “mtumwa mwaminifu mwenye akili.” (Mathayo 24:45-47) Je! ndivyo ilivyo kwetu sisi mmoja mmoja? Kama Noa, je! sisi tunajifunza kufanya ‘yote anayotuamuru Yehova’ na kufanya mambo kwa njia yake? (Mwanzo 6:22) Ikiwa ndivyo, tunaitikia utayarishaji ambao Yehova anatupatia kwa ajili ya ukombozi kuingia ndani ya ulimwengu wake mpya wenye uadilifu.

19. (a) Moyo wetu wa kitamathali ni nini, na kwa nini ni muhimu tuutolee uangalifu? (Mithali 4:23) (b) Tunaweza kunufaikaje kutokana na kielelezo cha Loti kwa habari ya itikio letu kuelekea vivutio vya ulimwengu?

19 Utayarishaji huo unahusu pia kutoa uangalifu kwa moyo wetu wa kitamathali. “Yehova ndiye mchunguzaji wa mioyo.” (Mithali 17:3, NW) Yeye hutusaidia tung’amue kwamba jambo la maana si vile tunavyoonekana nje-nje, bali ni mtu wa ndani-ndani, moyo. Ingawa hatujitii katika jeuri au hatushiriki mwendo wao wa ukosefu wa adili kama ulimwengu unaotuzunguka, tunahitaji kujilinda dhidi ya kuvutwa au kufurahishwa na mambo hayo. Kama Loti, twapaswa kuhisi tukisumbuliwa na kuwako kwenyewe kwa matendo hayo ya kuasi sheria. Wale wanaochukia yaliyo mabaya hawatakuwa wakitafuta njia za kujitia sana katika hayo; hata hivyo, huenda watu wasioyachukia wakajiepusha nayo kimwili lakini kiakili wakiona ni laiti wangeweza kushiriki. “O nyinyi wapenda Yehova, chukieni lililo baya.”—Zaburi 97:10, NW.

20. (a) Ni katika njia gani Biblia hutuonya dhidi ya njia ya maisha ya ufuatiaji vitu vya kimwili? (b) Tunaweza kujuaje kama masomo muhimu ya Biblia juu ya ufuatiaji vitu vya kimwili yameshikwa na moyo wetu?

20 Kwa upendo Yehova anatuelimisha tujiepushe si na mwenendo wa ukosefu wa adili tu bali pia na njia ya maisha ya ufuatiaji vitu vya kimwili. ‘Ridhika na chakula na nguo,’ Neno lake lashauri. (1 Timotheo 6:8) Ilikuwa lazima Noa na wanae waache nyuma makao yao walipoingia ndani ya safina. Pia, Loti na jamaa yake waliacha makao na mali yao ili waokoe uhai wao. Shauku zetu zimekazwa juu ya nini? “Kumbukeni mke wa Loti.” (Luka 17:32, NW) Yesu alihimiza hivi: “Fulizeni, basi, kutafuta kwanza ufalme na uadilifu wake.” (Mathayo 6:33, NW) Tunafanya hivyo? Ikiwa viwango vya uadilifu vya Yehova vinatuongoza na ikiwa kupiga mbiu ya habari njema za Ufalme wake ndilo hangaiko la kwanza maishani mwetu, basi sisi, tunaitikia kweli kweli utayarishaji wake wa kikundi cha watu kwa ajili ya ukombozi kuingia ndani ya ulimwengu wake mpya.

21. Kwa nini kwa kufaa tunaweza kutazamia kwamba ahadi ya Yehova ya ukombozi itatimizwa karibuni?

21 Kwa watu wa ujitoaji kimungu ambao wangeona utimizo wa ishara ya kuwapo kwake katika mamlaka ya Ufalme, Yesu alisema hivi: “Changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia.” (Luka 21:28) Je! wewe umeona ishara hiyo kadiri imekuwa ikitukia katika kila jambo dogo layo? Basi uwe na uhakika kwamba utimizo wa ahadi ya Yehova ya ukombozi u karibu sana! Usadikishwe kabisa kwamba “Yehova ajua kukomboa watu wa ujitoaji kimungu katika jaribu.”—2 Petro 2:9, NW.

Wewe Umejifunza Nini?

◻ Kama Loti, twapaswa kuitikiaje njia ya maisha ya ulimwengu?

◻Ni mitihani gani waliyokabili Loti na jamaa yake hata walipokuwa wakikimbia Sodoma?

◻ Vielelezo alivyotumia Petro hukaziaje uharaka wa kuchukua msimamo imara upande wa Yehova sasa?

◻ Katika kutayarisha watu wake kwa ajili ya ukombozi, ni masomo gani muhimu anayofundisha Yehova?

[Picha katika ukurasa wa 18]

Watu wa Mungu wanalindwa salama naye kama vile vifaranga chini ya mabawa yenye nguvu ya ndege mzazi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki