Toa kwa Ujasiri Mwaliko “Njoo!”
1 Matukio yenye kwenda kasi ulimwenguni pote huzitambulisha nyakati hizi kuwa “siku za mwisho.” (2 Tim. 3:1-5) Kupanda kwa uhalifu, ukosefu wa imara wa kiuchumi, na magonjwa yenye kutisha uhai ni mambo ambayo yameongeza mkazo wayo. Lakini kwa furaha, katika kuelekeana na ole hizo, watu wanatolewa mwaliko ambao ungeweza kuwaathiri kwa umilele. Roho na bibi-arusi huendelea kusema: “Njoo!” Na sasa “mkutano mkubwa” umejiunga nao katika kutoa mwaliko kwa watu wote kila mahali waje na kutwaa maji ya uhai bure.—Ufu. 7:9; 22:17.
2 Leo, wale wanaoona kiu kwa ajili ya uadilifu wanaitikia mwaliko huo kwa hesabu kubwa. Mwaka jana mamilioni walihudhuria mikusanyiko ya wilaya iliyofanywa ulimwenguni pote, na karibu milioni kumi walikuwapo kwenye Ukumbusho. Mamilioni ya wengine wanaonyesha uthamini wao kwa maandalizi ya Yehova kwa kusikiliza ujumbe wa Ufalme. Basi, ni jambo la maana kama nini kwamba, tutumie wakati wetu kwa hekima katika kutoa mwaliko huo waziwazi na nyumba kwa nyumba!—Mdo. 5:42; Efe. 5:15, 16.
SHIRIKI KWA UJASIRI
3 Wakristo wa mapema zaidi walinyanyaswa kwa kuhubiri kwa bidii. (Mdo. 16:19-21; 17:2-8) Hata hivyo, waliendelea na jitihada zao za kutangaza habari njema. Sisi vivyo hivyo lazima tuwe wajasiri na wenye kuazimia katika jitihada zetu za kuona kwamba habari njema zimehubiriwa.
4 Hata katika nchi ambako kazi imepigwa marufuku, akina ndugu wanashiriki kwa moyo wote katika kazi ya kuhubiri ijapokuwa mateso makali, kutia na uwezekano wa kupoteza kazi, makao, na hata uhuru wao. Kielelezo chao chema hutumika kuwa kitia-moyo kwetu tuendelee kuwaalika wengine “Njoo!”—2 The. 3:9.
5 Kwa miaka zaidi ya 35 baada ya kujifunza kweli, dada mmoja alidumisha tamaa ya moyoni ya kuwa painia. Hali zake za kibinafsi zilibadilika alipokuwa na umri wa miaka 70, naye akawa painia wa kawaida. Ijapokuwa ni watu wachache katika umri huo wangeingia katika kazi mpya ya maisha, yeye alifanya hivyo. Akiwa amekwisha kuonea shangwe huduma ya wakati wote sasa kwa hesabu fulani ya miaka, yeye husema, “Inakuwa nzuri kila siku.” Amewaletea wengine burudisho la kiroho kwa sababu ya kukubali bila hofu mwaliko wa Yehova afikilie na kushiriki kikamilifu utumishi wa Ufalme.
6 Kama ilivyokuwa katika karne ya kwanza, watu leo wanaitikia mwaliko huu, wakigeuza kufikiri kwao, wakibadili akili zao, na kuacha mazoea yenye kumvunjia Mungu heshima. Wanakuwa sehemu ya udugu wa kimataifa ulio wakfu wa Mashahidi na kujiunga na roho na bibi-arusi katika kusema “Njoo!” kwa watu wengine zaidi wenye mioyo minyofu.
7 Ongezeko kubwa mno katika kazi ya Ufalme na mpanuko wa ofisi za tawi katika nchi mbalimbali ni ushuhuda wa baraka za Yehova. Lakini wakati unaishia huu mfumo wa kale. Sasa ndio wakati ufaao wa kuonyesha ujasiri na bidii katika kutoa mwaliko “Njoo!” ili kwamba wengine waweze kuitikia kwa haraka na kutenda juu ya yale yanayosikiwa.—Mdo. 20:26, 27; Rum. 12:11.