Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/15 uku. 4
  • Mwaliko wa Moja kwa Moja

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mwaliko wa Moja kwa Moja
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Mwaliko wa Pekee
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Kampeni Ambayo Huwa na Matokeo Mazuri
    Huduma ya Ufalme—2013
  • Kampeni ya Kusambaza Mialiko ya Kusanyiko
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo (2016)
  • Usambazaji wa Mialiko ya Ukumbusho Utaanza Aprili 2
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2015
km 6/15 uku. 4

Mwaliko wa Moja kwa Moja

1. Kampeni ya kuwaalika watu kwenye kusanyiko itaanza lini?

1 Ikiwa unapanga kutayarisha mlo maalumu kwa ajili ya familia au marafiki, na utatumia gharama na jitihada nyingi, bila shaka utawakaribisha wageni wako kwa shauku. Vivyo hivyo, kazi nyingi zimefanywa ili kuandaa karamu ya kiroho kwenye kusanyiko lijalo la eneo. Majuma matatu kabla ya kusanyiko letu, tutakuwa na pendeleo la kuwaalika wengine wahudhurie. Ni nini kitakachotusaidia kuwaalika watu kwa shauku?

2. Ni nini kitakachotuchochea kushiriki katika kampeni kwa bidii?

2 Tukithamini jinsi tunavyofaidika kibinafsi kutokana na ufundishaji wenye kuburudisha ambao Yehova anatuandalia kwenye makusanyiko yetu, tutachochewa kushiriki katika kampeni hiyo kwa bidii. (Isa. 65:13, 14) Pia, tunapaswa kukumbuka kwamba kushiriki katika kampeni hiyo ya kila mwaka huleta matokeo mazuri. (Ona sanduku “Kampeni Huwa na Matokeo Mazuri.”) Baadhi ya wale ambao tutawakaribisha watahudhuria, ilhali wengine hawatahudhuria. Jitihada zetu wakati wa kampeni zitamletea Yehova sifa na kuonyesha jinsi alivyo mkarimu, haidhuru ni watu wangapi watahudhuria.—Zab. 145:3, 7; Ufu. 22:17.

3. Mialiko itasambazwaje?

3 Kila baraza la wazee linapaswa kuamua jinsi wahubiri katika makutaniko yao watakavyosambaza mialiko kwa watu wengi iwezekanavyo, kutia ndani iwapo wataacha mialiko hiyo katika nyumba ambazo wanawakosa watu au wataitoa wanapohubiri hadharani. Iwapo inafaa, mwisho-juma tunapaswa kutoa magazeti pamoja na mialiko. Mwishoni mwa kampeni hiyo tutafurahi sana kujua kwamba tulishiriki kwa bidii na shauku kuwaalika watu wengi iwezekanavyo ili wajiunge nasi katika karamu ya kiroho ambayo Yehova ametuandalia!

Utasema Nini?

Baada ya salamu, unaweza kusema hivi: “Tunashiriki katika kampeni inayofanywa ulimwenguni pote ya kuwaalika watu wahudhurie tukio muhimu sana. Mwaliko huu unaonyesha tarehe, wakati, na mahali pa tukio hilo.”

Kampeni Huwa na Matokeo Mazuri

  • Miaka kadhaa iliyopita, dada mmoja alipokuwa akishiriki katika kampeni ya kuwaalika watu kwenye kusanyiko alijiuliza ikiwa kuna faida ya kufanya jitihada zote hizo. Hata akajiuliza hivi, ‘Je, kweli watu watakubali mwaliko na kuhudhuria kusanyiko pamoja nasi?’ Jumamosi asubuhi siku ya kusanyiko, alimwona mwanamume Kalasinga ameketi karibu naye, hivyo akaamua kujitambulisha kwake. Alitambua kwamba alikuwa amehudhuria kusanyiko kwa sababu alipewa mwaliko. Alikuwa na maswali kadhaa ambayo dada huyo aliweza kuyajibu. Mwanamume huyo alieleza kwamba alifurahia programu na kuvutiwa na mwenendo wa wahudhuriaji na jinsi walivyovalia. Baadaye, siku hiyohiyo, dada huyo alianzisha mazungumzo na wenzi wa ndoa waliokuwa wameketi karibu naye. Wao pia walikuwa wamepokea mwaliko na walisafiri kwa basi ili kufika kusanyikoni. Walifurahia kusanyiko na wakapanga kuhudhuria mkutano siku ya Jumapili. Hivyo, dada huyo akatambua umuhimu wa kampeni yetu ya kila mwaka.

  • Walipokuwa katika kusanyiko moja lililofanywa hivi karibuni, wenzi wa ndoa ambao ni mapainia wa kawaida walijitambulisha kwa wenzi wa ndoa wenye umri mkubwa. Wenzi hao walisema kwamba hilo lilikuwa kusanyiko lao la kwanza kuhudhuria. Mapainia hao wakawauliza, “Ni nani aliyewaalika?” Wakajibu, “Siku moja tuliporudi nyumbani, tulikuta mwaliko chini ya mlango wa nyumba yetu.” Walisoma mwaliko huo na hata wakajaza sehemu iliyo nyuma ya mwaliko huo. Wahudhuriaji wengine katika kusanyiko hilo waliwaalika wale chakula cha mchana pamoja nao. Walifurahia sana programu na wakapanga kuhudhuria siku iliyofuata. Mipango ilifanywa ili watembelewe na kuendeleza mazungumzo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki