Usambazaji wa Mialiko ya Ukumbusho Utaanza Aprili 2
1. Mwaka huu, tutasambaza mialiko ya Ukumbusho lini, na kwa nini kampeni hii ya kila mwaka ni umuhimu?
1 Kuanzia Aprili 2 hadi Aprili 17, tutasambaza mialiko ya tukio muhimu zaidi katika mwaka, yaani, Ukumbusho wa kifo cha Kristo. Katika miaka iliyopita, watu wengi wanaopendezwa walikubali mwaliko wa kuhudhuria Ukumbusho. Kwa mfano, siku ya Ukumbusho mwaka fulani, mwanamke mmoja aliipigia ofisi ya tawi simu na akasema: “Nimefika nyumbani sasa hivi, na nikapata mwaliko ulioingizwa chini ya mlango nyumbani kwangu. Ninataka kuhudhuria, lakini sijui saa hususa.” Ndugu alimweleza mahali ambapo saa imeandikwa kwenye mwaliko. Mwanamke huyo alimalizia mazungumzo kwa kusema, “Nitahudhuria maadhimisho yenu jioni hii!”
2. Tunaweza kusema nini tunapompa mtu mwaliko?
2 Tutakavyoisambaza: Kwa kuwa tuna muda mfupi tu wa kusambaza mialiko, ni vizuri kuzungumza kifupi. Tunaweza kusema hivi: “Jambo. Tunataka kuwaalika watu wote wa familia yenu mhudhurie tukio muhimu ambalo huadhimishwa kila mwaka duniani kote. Mwaka huu tukio hilo litaadhimishwa Jumapili, Aprili 17. [Mpe mwenye nyumba mwaliko.] Tarehe hiyo ni siku ya kuadhimisha kifo cha Yesu. Hotuba inayoeleza jinsi tunavyonufaika na fidia ya Kristo itatolewa bila malipo. Karatasi hii ya mwaliko inaonyesha anwani na saa ya maadhimisho hayo katika eneo letu.”
3. Tunaweza kuwaalika watu wengi iwezekanavyo kwa njia gani?
3 Iwapo kutaniko lina eneo kubwa, huenda wazee wakawaagiza wahubiri waache mialiko katika nyumba zisizo na watu, lakini lazima iwekwe mahali ambapo wapita njia hawawezi kuiona. Usisahau kuwaalika watu wanaopendezwa unaowarudia mara kwa mara, watu wa ukoo, wafanyakazi wenzako, wanafunzi wenzako, na watu wengine unaowafahamu. Unaposhiriki kusambaza mialiko mwishoni mwa juma, watolee watu magazeti ikiwa inafaa. Je, unaweza kuwa painia msaidizi mwezi wa Aprili na kufurahia kushiriki kwa kiwango kikubwa zaidi katika kampeni hii?
4. Kwa nini tunataka watu wanaopendezwa wahudhurie Ukumbusho?
4 Watu wanaopendezwa watakaohudhuria watatolewa ushahidi mzuri sana! Watasikia kuhusu upendo mkuu wa Yehova uliofanya aandae fidia. (Yoh. 3:16) Watajifunza kuhusu manufaa ambazo Ufalme wa Mungu utawaletea wanadamu. (Isa. 65:21-23) Wataelezwa pia kwamba wanaweza kuwaendea wakaribishaji na kuomba funzo la Biblia ili wajifunze mengi zaidi. Ni matumaini yetu kwamba watu wengi wanaotaka kumjua Yehova watakubali mwaliko na kuhudhuria Ukumbusho pamoja nasi!