Kampeni ya Kuwaalika Watu Kwenye Ukumbusho Itaanza Machi 22
Mwaka huu kampeni ya kuwaalika watu kuhudhuria Ukumbusho inaanza Jumamosi, Machi 22. Wote wanatiwa moyo kushiriki kikamili. Katika miisho-juma tutatoa mialiko pamoja na magazeti ya karibuni inapofaa. Katika Jumamosi ya kwanza ya mwezi wa Aprili, tutakazia fikira kugawanya mialiko badala ya kuanzisha mafunzo ya Biblia. Hata hivyo, tunapompata mtu anayeonyesha upendezi, bado tunaweza kujaribu kuanzisha funzo la Biblia. Mwangalizi wa utumishi anaweza kuamua ikiwa kugawanya mialiko kwa kushiriki katika mahubiri ya hadharani kunaweza kusaidia kutaniko liwafikie watu wengi zaidi katika eneo. Anza sasa kuorodhesha majina ya watu wa ukoo, wafanyakazi wenzako, wanashule wenzako, watu wanaopendezwa na wengine unaowafahamu ambao ungependa kuwaalika na uwape mialiko kampeni inapoanza. Tunatumaini kwamba wengi wataungana nasi tunapoadhimisha upendo mkubwa zaidi ambao Yehova na Yesu walituonyesha.—Yohana. 3:16; 15:13.