Nchi Zinazotajwa Katika Biblia
TAIFA la Israeli lilipokuwa likijitayarisha kuingia katika Nchi ya Ahadi, Musa alimweleza Mungu tamaa yake kubwa kwa kusema: “Acha nivuke, tafadhali, niione hiyo nchi nzuri iliyo ng’ambo ya Yordani.”—Kum 3:25.
Musa hakuruhusiwa kuingia katika Nchi ya Ahadi, lakini alipanda mlima ulioelekeana na Yeriko na kuiona nchi hiyo—‘Gileadi mpaka Dani na nchi yote ya Yuda mpaka bahari ya magharibi na Negebu na uwanja wa bonde la Yordani.’ (Kum 3:27; 34:1-4) Je, umewahi kusikia majina hayo? Je, unajua maeneo hayo yako wapi?
Leo, ni watu wachache sana miongoni mwa watu wa Yehova wanaoweza kutembelea maeneo yanayotajwa katika Biblia. Hawawezi kufanya jambo ambalo Mungu alisema Abrahamu angefanya, yaani kusafiri kwa mapana na marefu katika Nchi ya Ahadi. (Mwa 13:14-17) Hata hivyo, Wakristo wa kweli wanatamani kujua maeneo yanayotajwa katika Biblia na kuona jinsi kila eneo linavyohusiana na lingine.
Broshua hii, ‘Ona Nchi Nzuri,’ inaweza kukusaidia kuyaelewa Maandiko vizuri zaidi. Ina picha za maeneo halisi, kama vile eneo la Gileadi ambalo limeonyeshwa kwenye jalada. Pia ramani zilizopo zinaweza kukusaidia sana kuelewa vizuri maeneo yanayotajwa katika Biblia.
Ramani iliyo kwenye ukurasa wa 2 na 3 inaonyesha maeneo au nchi kubwa-kubwa. Kwa mfano, ukijua Ashuru na Misri zilikuwa umbali gani kutoka Nchi ya Ahadi, utaweza kuelewa vizuri zaidi unabii unaotaja nchi hizo. (Isa 7:18; 27:13; Ho 11:11; Mik 7:12) Ukanda mdogo wa ardhi ambao uliitwa Nchi ya Ahadi ulikuwa kwenye makutano ya njia mbalimbali zilizotumiwa na wafanyabiashara, na mataifa mengine yalitaka kumiliki mashamba yake yenye rutuba ambapo nafaka, mizabibu, na mizeituni ilikuzwa.—Kum 8:8; Amu 15:5.
Huenda nyakati nyingine ukataka kulinganisha ramani mbalimbali. Kwa mfano, Yona alipewa mgawo wa kwenda jiji kuu la Ashuru, lakini akasafiri kwa meli hadi Tarshishi. (Yon 1:1-3) Je, unaona maeneo hayo kwenye ramani ya kwanza? Hata hivyo, usidhani kwamba Tarshishi ni Tarso, mahali alipozaliwa mtume Paulo. Utaona Tarso na majiji mengine mashuhuri kwenye ramani unayoona hapa.
Fikiria umbali na pia njia ambayo Abrahamu alifuata unapotafuta majiji ya Uru, Harani, na Yerusalemu. Baada ya Yehova kumwita kutoka Uru, Abrahamu aliishi Harani kisha akahamia Nchi ya Ahadi. (Mwa 11:28–12:1; Mdo 7:2-5) Utafahamu vizuri zaidi safari ya Abrahamu unapochunguza “Maeneo Walikoishi Wazee wa Ukoo,” kwenye ukurasa wa 6-7.
Ramani ya kwanza na ile unayoona hapa hazihusu kipindi fulani hususa. Baada ya ramani hizo mbili, ramani nyinginezo zinafuata mpangilio wa matukio katika historia. Majiji au habari nyinginezo katika ramani zinaonyesha matukio ya wakati hususa. Ingawa Faharisi (ukurasa wa 34-35) haitaji kila eneo lililo katika ramani, inaweza kukusaidia kupata ramani zenye habari unayotafuta.
Ramani iliyo kwenye kurasa za katikati (ukurasa wa 18-19) ndiyo yenye miji na majiji mengi zaidi katika Nchi ya Ahadi. Ufunguo wa Ramani utakusaidia kupata miji ya Walawi na ile miji sita ya makimbilio, na vilevile kujua iwapo eneo fulani lilitajwa katika Maandiko ya Kiebrania, ya Kigiriki, au katika Maandiko yote mawili.
Leo, maeneo fulani yanayotajwa katika Biblia hayajulikani yalikuwa wapi, kwa hiyo mengi ya majina hayo hayako katika ramani iliyo kwenye kurasa za katikati. Pia, haingewezekana kuonyesha kila mji na jiji. Kwa mfano, haingewezekana kuonyesha miji yote inayotajwa katika orodha ya mipaka ya makabila. (Yos, sura ya 15-19) Hata hivyo, ramani hiyo inaonyesha majiji yaliyokuwa karibu na mipaka hiyo, na hivyo inakuwezesha kukisia mahali miji hiyo ilipokuwa. Kuna alama zinazoonyesha sura ya nchi (milima, mito, na mabonde ya mto), na rangi mbalimbali zimetumiwa kuonyesha sehemu tambarare na zilizoinuka. Habari hizo zinaweza kukusaidia upige picha akilini kuhusu matukio yanayotajwa katika Biblia.
Unaweza kupata habari zaidi kuhusu maeneo yanayotajwa katika Biblia katika kitabu Insight on the Scriptures, ambacho kimechapishwa katika lugha nyingi.a Unapotumia kitabu hicho pamoja na vitabu vingine vya kukusaidia kujifunza Biblia, iweke karibu broshua ‘Ona Nchi Nzuri.’ Tumia broshua hiyo unaposoma Maandiko yote, na hayo yananufaisha sana maishani.—2Ti 3:16, 17.
[Maelezo ya Chini]
a Kimechapishwa na Mashahidi wa Yehova.
[Sanduku katika ukurasa wa 5]
VITABU VYA BIBLIA VILIANDIKWA HUKO
Babiloni
Efeso
Kaisaria
Korintho
Makedonia
Misri
Moabu
Nchi ya Ahadi
Patmo
Roma
Shushani
Yerusalemu
[Ramani katika ukurasa wa 4, 5]
(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)
Nchi za Biblia na Miji Mikuu
A1 ITALIA
A2 ROMA
A3 SISILI
A3 MALTA
C2 MAKEDONIA
C2 Filipi
C2 UGIRIKI
C3 ATHENE
C3 Korintho
C3 KRETE
C4 LIBYA
D3 Antiokia (ya Pisidia)
D3 Efeso
D3 PATMO
D3 RODE
D4 MEMFISI
D5 MISRI
E2 ASIA NDOGO
E3 Tarso
E3 Antiokia (ya Siria)
E3 KIPRO
E4 Sidoni
E4 Damasko
E4 Tiro
E4 Kaisaria
E4 NCHI YA AHADI
E4 YERUSALEMU
E4 MOABU
E4 Kadeshi
E4 EDOMU
F3 Bustani ya Edeni?
F3 ASHURU
F3 Harani
F3 SIRIA
F5 ARABIA
G3 NINAWI
G4 BABILONI
G4 UKALDAYO
G4 Shushani
G4 Uru
H3 UMEDI
[Milima]
E5 Ml. Sinai
G2 MIL. YA ARARATI
[Bahari]
C3 Bahari ya Mediterania (Bahari Kuu)
E1 Bahari Nyeusi
E5 Bahari Nyekundu
H2 Bahari ya Kaspian
H5 Ghuba ya Uajemi
[Mito]
D5 Mto Nile
F3 Mto Efrati
G3 Mto Tigri