Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • gl kur. 24-25
  • Watu Wa Mungu Warudi Nchini Kwao

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Watu Wa Mungu Warudi Nchini Kwao
  • ‘Ona Nchi Nzuri’
  • Habari Zinazolingana
  • Wayahudi Waathiriwa Na Utawala Wa Wagiriki Na Waroma
    ‘Ona Nchi Nzuri’
  • Nchi Zinazotajwa Katika Biblia
    ‘Ona Nchi Nzuri’
  • Falme Zashambulia Nchi Ya Ahadi
    ‘Ona Nchi Nzuri’
  • Umedi-Uajemi—Ile Serikali Kubwa ya Nne ya Ulimwengu Katika Historia ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Pata Habari Zaidi
‘Ona Nchi Nzuri’
gl kur. 24-25

Watu Wa Mungu Warudi Nchini Kwao

Milki ya Umedi na Uajemi

SAFU mbili za milima mirefu—Elburzi (kusini ya Bahari ya Kaspian) na Zagro (kusini-mashariki ya Ghuba ya Uajemi) zinazunguka uwanda wa juu ulio katika eneo lililo katika Irani ya sasa. Mabonde ya milima hiyo yana udongo wenye rutuba na miteremko yake ina miti mingi. Mabonde hayo yana tabia ya nchi yenye kupendeza, lakini maeneo tambarare ya milima hiyo ni makame na huwa baridi sana wakati wa majira ya baridi kali. Karibu na maeneo hayo tambarare kuna jangwa linalokaliwa na watu wachache. Milki ya Umedi na Uajemi ambayo iliibuka kuwa serikali kubwa ya ulimwengu ilikuwa katika eneo hilo lililo mashariki ya Mesopotamia.

Wamedi waliishi hasa kwenye eneo lililo kaskazini mwa uwanda huo wa juu, ijapokuwa baadaye walisambaa hadi Armenia na Kilikia. Hata hivyo, Waajemi waliishi kusini-magharibi mwa uwanda huo wa juu, mashariki ya Bonde la Tigri. Katikati ya karne ya sita K.W.K., wakati wa utawala wa Koreshi, falme hizo mbili ziliungana na kuwa Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Umedi na Uajemi.

Koreshi aliteka Babiloni mwaka wa 539 K.W.K. Milki yake ilienea upande wa mashariki hadi India na upande wa magharibi hadi Misri na eneo ambalo ni Uturuki ya sasa. Kwa kufaa, Danieli alifafanua Milki ya Umedi na Uajemi kuwa kama “dubu” mwenye tamaa ‘aliyekula nyama nyingi.’ (Da 7:5) Koreshi aliwavumilia na kuwahurumia watu aliowatawala. Aligawanya milki hiyo katika mikoa mbalimbali. Kila mkoa ulitawaliwa na liwali ambaye kwa kawaida alikuwa Mwajemi, lakini chini yake kulikuwa na mtawala mwenyeji aliyekuwa na mamlaka fulani. Raia wa miliki hiyo ambao walitoka mataifa na makabila mbalimbali walitiwa moyo waendelee na dini na desturi zao.

Kupatana na sera hiyo, Koreshi aliwaruhusu Wayahudi warudi kwao na kuanzisha tena ibada ya kweli na kujenga Yerusalemu, kama inavyoelezwa na Ezra na Nehemia. Unafikiri kundi hilo kubwa la watu walipitia wapi walipokuwa wakirudi kwao? Je, walitumia njia aliyotumia Abrahamu kwa kupitia upande wa juu wa Mto Efrati hadi Karkemishi au labda walitumia njia fupi zaidi kupitia Tadmori na Damasko? Biblia haielezi jambo hilo. (Ona ukurasa wa 6-7.) Baada ya muda, Wayahudi walianza kuishi sehemu nyingine za milki hiyo, kama vile kwenye Delta ya Nile na sehemu zilizo upande wa kusini kabisa. Wayahudi kadhaa waliendelea kuishi Babiloni, na yaelekea hiyo ndiyo sababu iliyofanya mtume Petro atembelee jiji hilo karne nyingi baadaye. (1Pe 5:13) Kwa kweli, Milki ya Umedi na Uajemi ilichangia sana kuwepo kwa Wayahudi katika sehemu nyingi wakati wa utawala uliofuata wa Wagiriki na Waroma.

Baada ya kuteka jiji la Babiloni, serikali ya Umedi na Uajemi ilitumia jiji hilo lenye majira yenye joto jingi kuwa kituo cha shughuli za serikali. Shushani, lililokuwa jiji kuu la Elamu hapo awali, lilikuwa mojawapo ya majiji ya kifalme. Baadaye, huko Shushani, Mfalme Ahasuero wa Uajemi (yaelekea ni Artashasta wa Kwanza) alimchagua Esta kuwa malkia wake na kuzuia njama ya kuangamiza watu wa Mungu katika milki hiyo kubwa. Majiji mengine mawili makuu ya milki ya Umedi na Uajemi yalikuwa Ekibatana (jiji lenye majira ya joto yenye kupendeza, lililokuwa zaidi ya meta 1,900 juu ya usawa wa bahari) na Pasargadae (lililokuwa zaidi ya meta 1,900 juu ya usawa wa bahari, karibu kilometa 650 kusini-mashariki ya Ekibatana).

Serikali hiyo kubwa ya ulimwengu iliporomokaje? Wakati serikali ya Umedi na Uajemi ilipokuwa imefikia upeo wa utawala wake, ilichukua hatua kumaliza uasi uliochochewa na Wagiriki kutoka mpaka wake wa kaskazini-magharibi. Wakati huo, nchi ya Ugiriki ilikuwa imegawanywa katika majiji yenye kujitawala yaliyokuwa yakipigana. Lakini majiji hayo yaliungana na kushinda majeshi ya Waajemi katika vita vya kufa na kupona huko Marathoni na Salami. Baada ya vita hivyo, Ugiriki iliyoungana iliibuka kuwa serikali kubwa ya ulimwengu.

[Sanduku katika ukurasa wa 25]

Chini ya utawala wa Zerubabeli, wanaume Waisraeli wapatao 50,000 walisafiri umbali wa kati ya kilometa 800 hadi 1,600 (ikitegemea njia waliyopitia) kurudi Yerusalemu. Walikabili hali ngumu sana ya kiuchumi. Nchi yao ilikuwa imeachwa ukiwa kwa miaka 70. Waisraeli waliorudi walianza kurudisha ibada ya kweli kwa kujenga madhabahu na kumtolea Yehova dhabihu. Katika mwezi wa Oktoba, mwaka wa 537 K.W.K., walisherehekea Sikukuu ya Vibanda. (Yer 25:11; 29:10) Kisha Waisraeli hao wakaweka msingi wa nyumba ya Yehova.

[Sanduku katika ukurasa wa 25]

VITABU VYA BIBLIA TANGU WAKATI HUO:

Danieli

Hagai

Zekaria

Esta

Zaburi (sehemu)

Mambo ya Nyakati 1 na 2

Ezra

Nehemia

Malaki

[Ramani katika ukurasa wa 24]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

Milki ya Umedi na Uajemi

A2 MAKEDONIA

A2 THRACE

A4 Kirene

A4 LIBYA

B2 Byzantiumu

B2 LIDIA

B3 Sardi

B4 Memfisi (Nofu)

B4 MISRI

B5 No-amoni (Thebesi)

B5 Sewene

C3 KILIKIA

C3 Tarso

C3 Iso

C3 Karkemishi

C3 Tadmori

C3 SIRIA

C3 Sidoni

C3 Damasko

C3 Tiro

C4 Yerusalemu

D2 Phasis

D2 ARMENIA

D3 ASSIRIA

D3 Ninawi

D4 Babiloni

E3 UMEDI

E3 Ekibatana (Akmetha)

E3 HYRCANIA

E4 Shushani (Susa)

E4 ELAMU

E4 Pasargadae

E4 Persepoli

E4 UAJEMI

F3 PARTHIA

F4 DRANGIANA

G2 Marakanda (Samarkandi)

G3 SOGDIANA

G3 BAKTRIA

G3 ARIA

G4 ARIACHOSIA

G4 GEDROSIA

H5 INDIA

[Mahali Pengine]

A2 UGIRIKI

A3 Marathoni

A3 Athene

A3 Salamisi

C1 SCYTHIA

C4 Elathi (Elothi)

C4 Tema

D4 ARABIA

[Milima]

E3 MIL. ELBURUSI

E4 MIL. ZAGROS

[Bahari na Ziwa]

B3 Bahari ya Mediterania (Bahari Kuu)

C2 Bahari Nyeusi

C5 Bahari Nyekundu

E2 Bahari ya Kaspian

E4 Ghuba ya Uajemin

[Mito]

B4 Nile

C3 Efrati

D3 Tigri

H4 Indus

[Picha katika ukurasa wa 24]

Majeshi ya Koreshi yalilazimika kuvuka Milima ya Zagro ili kufika Babiloni

[Picha katika ukurasa wa 25]

Juu: Lango la Mataifa Yote huko Persepoli

[Picha katika ukurasa wa 25]

Picha ndogo: Kaburi la Koreshi huko Pasargadae

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki