Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • jl somo la 11
  • Kwa Nini Tunahudhuria Makusanyiko?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Tunahudhuria Makusanyiko?
  • Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Habari Zinazolingana
  • Kufurahi na Kumsifu Mungu Kwenye Makusanyiko
    Mashahidi wa Yehova—Wanafanya Mapenzi ya Mungu kwa Umoja Ulimwenguni Pote
  • Mikutano ‘Inayotuchochea Katika Upendo na Matendo Mazuri’
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
jl somo la 11

SOMO LA 11

Kwa Nini Tunahudhuria Makusanyiko?

Kusanyiko la eneo la Mashahidi wa Yehova nchini Mexico

Mexico

Chapisho likitolewa kwenye kusanyiko la eneo nchini Ujerumani

Ujerumani

Mashahidi wa Yehova wakiwa katika kusanyiko la eneo nchini Botswana

Botswana

Kijana akibatizwa nchini Nikaragua

Nikaragua

Drama ikiigizwa kwenye kusanyiko la eneo nchini Italia

Italia

Kwa nini watu hawa wana furaha? Wamehudhuria mojawapo ya makusanyiko yetu. Kama watumishi wa Mungu wa wakati uliopita ambao waliagizwa wakusanyike mara tatu kwa mwaka, sisi pia hutazamia kwa hamu kukusanyika pamoja katika makusanyiko. (Kumbukumbu la Torati 16:16) Kila mwaka tuna makusanyiko matatu: makusanyiko mawili ya mzunguko, kila kusanyiko kwa siku moja, na kusanyiko la eneo linalofanywa kwa siku tatu. Tunafaidika jinsi gani kwa kuhudhuria makusanyiko hayo?

Yanaimarisha ushirika wetu wa Kikristo. Kama vile Waisraeli walivyoshangilia kumsifu Yehova katika “makusanyiko,” sisi pia hushangilia kumwabudu Yehova katika makusanyiko. (Zaburi 26:12, maelezo ya chini; 111:1) Makusanyiko hutuwezesha kukutana na kushirikiana na Mashahidi wenzetu wa makutaniko mengine au hata nchi nyingine. Wakati wa mchana, tunafurahia kula pamoja mahali pa kusanyiko, jambo linalochangia mazingira ya kirafiki katika pindi hizo za kiroho. (Matendo 2:42) Katika makusanyiko tunajionea upendo unaotuunganisha tukiwa “ushirika mzima wa akina ndugu” ulimwenguni pote.—1 Petro 2:17.

Yanatusaidia kufanya maendeleo ya kiroho. Waisraeli walifaidika pia kwa ‘kuelewa maneno’ ya Maandiko yaliyokuwa yakifafanuliwa mbele yao. (Nehemia 8:8, 12) Sisi pia tunathamini mafundisho ya Biblia tunayopokea katika makusanyiko yetu. Kila programu hutegemea habari za Kimaandiko. Kupitia hotuba zenye kusisimua, mifululizo, na maigizo, tunafundishwa jinsi ya kufanya mapenzi ya Mungu katika maisha yetu. Tunatiwa moyo tunaposikia masimulizi ya wale ambao wamefaulu kubaki waaminifu licha ya hali ngumu. Kwenye makusanyiko ya eneo, drama hutusaidia kuona kihalisi masimulizi ya Biblia na kutufundisha masomo muhimu. Katika kila kusanyiko, wale ambao wamejiweka wakfu kwa Mungu na wangependa kubatizwa, hubatizwa.

  • Kwa nini makusanyiko ni pindi zenye furaha?

  • Unaweza kufaidika jinsi gani kwa kuhudhuria kusanyiko?

PATA KUJUA MENGI ZAIDI

Ikiwa ungependa kutujua vizuri zaidi, tafadhali hudhuria kusanyiko letu lijalo. Yule anayejifunza Biblia pamoja na wewe anaweza kukuonyesha programu ya kusanyiko ili uone habari zitakazozungumziwa. Tia alama kwenye kalenda yako tarehe na mahali ambapo kusanyiko lijalo litafanywa, na ujitahidi kuhudhuria.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki