Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • je kur. 18-19
  • Kufurahi na Kumsifu Mungu Kwenye Makusanyiko

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kufurahi na Kumsifu Mungu Kwenye Makusanyiko
  • Mashahidi wa Yehova—Wanafanya Mapenzi ya Mungu kwa Umoja Ulimwenguni Pote
  • Habari Zinazolingana
  • Mikusanyiko Uthibitisho wa Udugu Wetu
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Yehova Anawakutanisha Watu Wake Wenye Shangwe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Mashahidi wa Yehova Watafanya Mikusanyiko ya Kimataifa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Makusanyiko ya Kila Mwaka—Fursa za Kuonyesha Upendo
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2021
Pata Habari Zaidi
Mashahidi wa Yehova—Wanafanya Mapenzi ya Mungu kwa Umoja Ulimwenguni Pote
je kur. 18-19

Kufurahi na Kumsifu Mungu Kwenye Makusanyiko

Tangu miaka ya mapema ya 1880 Wanafunzi wa Biblia waliona kwamba, zaidi ya mikutano ya kundi, lingekuwa jambo la faida kwao wajuane sana na waamini wenzao kutoka maeneo mengine. Hivyo walianza kupanga mikusanyiko ya kila mwaka ya Wanafunzi wa Biblia kutoka United States yote, na baadaye kutoka Kanada. Hivyo vilikuwa vipindi vya burudisho la kiroho; kwa siku kadha maagizo mengi ya Biblia yalitolewa, na wote walifurahia kutiana moyo kwa njia ya kupendeza sana. Ubatizo wa waamini wapya ukawa sehemu ya kawaida kwenye mikusanyiko. Mikusanyiko ilitumiwa pia kutoa ushuhuda ulio mkubwa zaidi kwa watu wengi. —Warumi 1:11, 12.

Leo Mashahidi wa Yehova wanafurahia makusanyiko ya kawaida. Kwa kawaida makundi karibu 18 mpaka 25 yanakusanywa pamoja katika ile inayoitwa, mizunguko inayotembelewa, au kutumikiwa, na waangalizi wasafirio. Mara mbili kwa mwaka, makusanyiko yanapangwa mahali ambako makundi katika mzunguko, au sehemu ya mzunguko huo, yanakutana pamoja Jumamosi na/au Jumapili.

Mara moja kila mwaka, mikusanyiko mikubwa zaidi ya siku tatu au nne, iitwayo mikusanyiko ya wilaya, inapangwa ifanywe katika kila nchi, ambamo maelfu wanaweza kukusanyika pamoja mahali pamoja. Mikusanyiko hiyo inatoa ujenzi wa kiroho kwa Mashahidi wa Yehova na wengine wanaopendezwa na utendaji wao, na pia inatoa ushuhuda kwa watu wengi.

Programu ya makusanyiko hayo na mikusanyiko hiyo inatayarishwa na Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova na inategemea mahitaji ya Mashahidi ulimwenguni pote. Ina hotuba, mazungumzo, na masimulizi ya kweli ya maisha yanayoitwa mawonyesho, yanayotolewa na waangalizi wasafirio na Mashahidi wenye kustahili kutoka makundi. Pia watu mbalimbali wanasimulia mambo waliyoona juu ya jinsi wanavyoshughulika na matatizo ya kuishi wakiwa Wakristo katika ulimwengu unaomkana Mungu au juu ya matokeo wanayopata katika huduma. Kwenye mikusanyiko ya wilaya kuna sehemu zaidi—masimulizi machangamfu kwa namna ya michezo ya kuigiza ya Biblia au michezo ya kuigiza ya hali za kisasa, yenye kuonyesha jinsi Wakristo wanavyopambana na matatizo wanayokabili leo.

Pia vyakula na viburudisho vinatolewa, kwa mchango mdogo. Hiyo inaruhusu kuwe ushirika wenye kufurahika wakati mikutano haiendelei. Kazi yote hiyo ya kutayarisha mambo hayo inafanywa na wenye kujitolea miongoni mwa Mashahidi wa Yehova. Gharama ya vifaa na gharama nyingine zinalipiwa kwa michango ya kujitolea. Kuingia ni bure, na hakuna sadaka zinazochukuliwa.

Unaweza kuchunguza mwenyewe kutoka kundi la mahali penu la Mashahidi wa Yehova ujue ni wakati gani na ni wapi makusanyiko hayo yamepangwa kufanywa katika eneo lenu. Taarifa itatolewa pia juu ya mipango yo yote ya kusafiri, na pia jinsi ya kupata malazi.

Makusanyiko hayo na mikusanyiko hiyo inasaidia Mashahidi wa Yehova na wote wanaoshirikiana nao wajue mengi kuliko yale yaliyo katika kundi lao na kuthamini ushirika mzima wa ndugu zao katika ulimwengu. —1 Petro 2:17.

• Ni faida gani ambazo Wanafunzi wa Biblia wa kwanza walipata kutokana na mikusanyiko yao?

• Simulia mpango na programu ya makusanyiko ya mizunguko na mikusanyiko ya wilaya.

[Picha katika ukurasa wa 18]

Mchezo wa Biblia, mkusanyiko, United States

Mkusanyiko wa kimataifa, Polandi

Mkusanyiko wa kimataifa, Argentina

Kusanyiko la mzunguko, Japani

Wajumbe wanapata vitabu, Uswisi

Ubatizo, Afrika Kusini

Kutolewa kwa kichapo kipya, Kanada

Wajumbe wanaimba, Hispania

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki