Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w97 4/1 uku. 29
  • Mashahidi wa Yehova Watafanya Mikusanyiko ya Kimataifa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mashahidi wa Yehova Watafanya Mikusanyiko ya Kimataifa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Habari Zinazolingana
  • Makusanyiko ya Kimataifa Katika Mwaka wa 2003
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Mikusanyiko Uthibitisho wa Udugu Wetu
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Kufurahi na Kumsifu Mungu Kwenye Makusanyiko
    Mashahidi wa Yehova—Wanafanya Mapenzi ya Mungu kwa Umoja Ulimwenguni Pote
  • Yehova Anawakutanisha Watu Wake Wenye Shangwe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
w97 4/1 uku. 29

Mashahidi wa Yehova Watafanya Mikusanyiko ya Kimataifa

Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova linapanga kufanya mikusanyiko ya kimataifa katika 1998. Tangazo hilo lilipokewa kwa itikio lenye idili kwenye mkutano wa kila mwaka wa Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania, uliofanywa katika Jumba la Kusanyiko la Jiji la Jersey siku ya Jumamosi, Oktoba 5, 1996.

Pamoja na mikusanyiko ya wilaya ya kawaida, mikusanyiko ya kimataifa kadhaa itafanywa Amerika Kaskazini katikati ya mwaka wa 1998. Yatarajiwa kwamba mikusanyiko hiyo itaunganisha mamia ya maelfu ya Mashahidi kutoka sehemu nyingi za dunia. Ili kuwezesha nchi nyingi iwezekanavyo kuwakilishwa, kila moja ya zile ofisi za tawi zaidi ya 100 za Watch Tower Society itakuwa na wajumbe kadhaa kwa ajili ya jiji hususa la mkusanyiko wa kimataifa katika Amerika Kaskazini.

Kwa wazi, si wote ambao wangependa kusafiri hadi Amerika Kaskazini watakaoweza kufanya hivyo. Hata hivyo, huenda ikawezekana kwa maelfu ya watu kuhudhuria mkusanyiko wa kimataifa karibu zaidi na kwao. Mipango inafanywa kwa ajili ya mikusanyiko ya kimataifa kufanywa katika nchi mbili au tatu za Ulaya na mingine katika Afrika, Asia, Amerika ya Latini, Pasifiki Kusini, na Karibea.

Kwenye wakati ufaao, ofisi za tawi za Sosaiti zitajulisha makutaniko katika maeneo yazo juu ya jiji au majiji ya mkusanyiko ambako yamealikwa. Habari juu ya tarehe mbalimbali za mkusanyiko na mipango ya kuwachagua wajumbe itatolewa. Wale wafikiriao kujaza fomu za maombi kwa ajili ya uteuzi wa wajumbe huenda wakataka kuanza kuhifadhi kiasi fulani cha fedha zao wakitarajia matukio hayo ya pekee.

Mashahidi wa Yehova wote ulimwenguni pote wanaweza kutazamia kilicho akibani kwenye mikusanyiko hiyo ya kimataifa ya mwaka wa 1998. Mikusanyiko ya wilaya katika nchi zote itakuwa na programu ileile.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki