Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • jl somo la 10
  • Ibada ya Familia Ni Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ibada ya Familia Ni Nini?
  • Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Habari Zinazolingana
  • Msaada kwa Familia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha​—Sehemu ya 2
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Mwabuduni Yehova Mkiwa Familia
    Unaweza Kuwa na Familia Yenye Furaha
  • Ibada ya Familia​—Je, Mnaweza Kuifanya Ifurahishe Zaidi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Pata Habari Zaidi
Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
jl somo la 10

SOMO LA 10

Ibada ya Familia Ni Nini?

Familia ikifurahia ibada ya familia

Korea Kusini

Wenzi wa ndoa wakijifunza Biblia

Brazili

Shahidi wa Yehova akijifunza Biblia

Australia

Familia ikijadili habari fulani katika Biblia

Guinea

Tangu nyakati za kale, Yehova alitaka kila familia iwe na wakati wa kuwa pamoja ili kuimarisha hali yao ya kiroho na vilevile kujenga uhusiano wa karibu miongoni mwao. (Kumbukumbu la Torati 6:6, 7) Ndiyo sababu Mashahidi wa Yehova wanatenga wakati kila juma kwa ajili ya ibada ya familia. Katika pindi hizo, wakiwa wamestarehe, wanazungumzia mambo ya kiroho yanayohusu familia zao. Hata ikiwa unaishi peke yako, unaweza kutumia wakati huo pamoja na Mungu kwa kujifunza jambo fulani katika Biblia.

Ni wakati wa kumkaribia Yehova. “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.” (Yakobo 4:8) Tunaweza kumjua Yehova vizuri hata zaidi tunapojifunza mambo hususa kuhusu utu wake na matendo yake kupitia Neno lake. Ikiwa hamna ibada ya familia, njia rahisi ya kuianzisha ni kusoma Biblia kwa sauti mkiwa pamoja. Labda mnaweza kutumia ratiba ya kila juma ya Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo. Mnaweza kusoma kwa zamu, kisha mzungumzie mambo mliyojifunza katika Maandiko.

Ni wakati wa kuimarisha uhusiano katika familia. Waume na wake, na vilevile wazazi na watoto, wanaweza kuimarisha uhusiano wao wanapojifunza Biblia pamoja wakiwa familia. Huo unapaswa kuwa wakati wa furaha na utulivu ambao kila mtu anatazamia kwa hamu kila juma. Ikitegemea umri wa watoto, wazazi wanaweza kuchagua habari zinazoifaa familia, labda makala ya Mnara wa Mlinzi au Amkeni! Mnaweza kuzungumzia matatizo ambayo watoto wenu walikabili shuleni na jinsi ya kuyashughulikia. Kwa nini msitazame Programu kwenye JW Broadcasting (tv.jw.org) na kisha muizungumzie pamoja? Mnaweza kufanya mazoezi ya nyimbo zitakazoimbwa katika mikutano na hata kuwa na viburudisho baada ya ibada ya familia.

Wakati huo wa pekee mnaotumia pamoja kila juma katika kumwabudu Yehova utamsaidia kila mmoja katika familia afurahie kujifunza Neno la Mungu, naye atabariki jitihada zenu.—Zaburi 1:1-3.

  • Kwa nini tunatenga wakati kwa ajili ya ibada ya familia?

  • Wazazi wanawezaje kufanya pindi hiyo iwe yenye kufurahisha?

PATA KUJUA MENGI ZAIDI

Waulize wengine kutanikoni mambo wanayofanya katika ibada ya familia. Pia, tafuta machapisho yanayopatikana katika Jumba la Ufalme ambayo unaweza kutumia kuwafundisha watoto wako kumhusu Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki